Jumanne, 16 Julai 2013

Kiongozi wa kundi la kuuza madawa ya kulevywa akamatwa

Serikali  nchini  Mexico  imethibitisha  kuwa  jeshi  lake  la majini  limemkamata  kiongozi  mkuu  wa  kundi linalotuhumiwa  kufanya  biashara  ya  madawa  ya kulevywa. Miguel  Angel Trevino  Morales,  kiongozi  wa kundi linalouza  madawa ya  kulevywa la  Zetas , amekamatwa   katika  mji  wa  Nuevo Laredo, ambao  uko katika  mpaka  na  jimbo  la  Texas  nchini  Marekani , pamoja  na  watu  wengine  wawili. 
Kundi  la  Zetas  liliundwa na  wanajeshi  wa  kikosi maalum na  linaonekana  kuwa  moja  kati  ya makundi yenye kuongopwa nchini  Mexico na yanayofanya uhalifu wa kupangiliwa .
Kukamatwa huko kunaelezwa kuwa  ni  hatua kubwa iliyopigwa na pigo  kubwa  kwa makundi  yanayofanya biashara ya  mihadarati nchini  Mexico, ambayo yanahusishwa  na ongezeko  la  matukio  ya  ghasia  na zaidi  ya  vifo 70,000  tangu  mwaka  2006.
Wizara  ya  mambo  ya  kigeni  ya  Marekani imetoa zawadi ya hadi  dola  milioni  tano  ili  kupata taarifa  zitakazosaidia kukamatwa  kwa  Trevino Morales.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni