Msichana wa Pakistan aliyepigwa risasi na Taliban nchini humo, Malala
Yousafzai, amesema kuwa siku ya malala duniani sio kwa ajili yake, bali ni
kwa ajili ya wanawake, wasichana na wavulana waliopaza sauti kutetea haki
zao. Malala ametoa kauli hiyo leo wakati akihutubia kwa mara ya kwanza
katika Baraza Kuu la Vijana la Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani.
Malala ambaye leo anatimiza miaka 16, alipigwa risasi kichwani na Taliban
mwezi Oktoba mwaka uliopita, baada ya kutetea haki ya watoto wa kike
kupatiwa elimu. Amesema kuwa silaha kubwa kwao ni vitabu na peni na
kwamba elimu ndio suluhisho pekee. Malala amemkabidhi Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, ombi lililosainiwa na karibu watu milioni nne
linalotaka kusaidiwa kwa watoto milioni 57 wasio na uwezo wa kwenda shule
pamoja na kuwafadhili walimu, shule na vitabu ili kufikia lengo la elimu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni