Mahakama moja nchini Romania, imemuhukumu waziri wa usafiri Relu
Fenechiu kifungo cha miaka mitano jela kutokana na rushwa. Fenechiu
amepatikana na hatia ya kuuza vifaa vya umeme vya mitumba kwa kampuni
ya nchi hiyo kwa gharama za vifaa vipya kati ya mwaka 2002 na 2005.
Waendesha mashtaka wamesema kuwa vifaa hivyo viligharimu Euro milioni
1.7. Fenechiu ambaye amekuwa akikanusha madai hayo na kukataa kuachia
madaraka, anakuwa waziri wa kwanza wa Romania kupewa adhabu ya
kifungo jela. Wakili wake amesema mteja wake atakata rufaa. Kwa mujibu wa
sheria za Romania, Fenechieu hatokwenda jela hadi rufaa yake
itakaposikilizwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni