Maafisa nchini Kenya wamesema kuwa afisa mmoja wa ubalozi wa
Marekani nchini humo ambaye alimuua raia mmoja wa Kenya baba wa watoto
watatu na kuwajeruhi wengine wanane katika ajali ya gari huko Nairobi,
ametoroka nchini humo. Maafisa wa Kenya wameripoti kuwa mwanadiplomasia
huyo wa Marekani kwa jina la Johsua Walde alikiuka sheria za barabarani
na kugonga gari la abiria aina ya matatu na kuua mtu mmoja na kuwajerhi
vibaya abiria wengine wanane Julai 11 mwaka huu. Baada ya kutokea ajali
hiyo, maafisa wa ubalozi wa Marekani mjini Nairobi siku iliyofuata
walimsafirisha nje ya nchi mwanadiplomasia huyo na familia yake.
Ubalozi wa Marekani mjini Nairobi baadaye ulitoa salamu za rambirambi kwa familia ya mhanga wa ajali hiyo. Hata hivyo haukutaja fidia yoyote utakayotoa kwa familia hiyo iliyosalia bila ya msaada wowote wa kifedha ili kugharamia shughuli za mazishi na gharama za hospitali kwa majeruhi wengine wa ajali hiyo iliyosababishwa na mwanadiplomasia wao.
Ubalozi wa Marekani mjini Nairobi baadaye ulitoa salamu za rambirambi kwa familia ya mhanga wa ajali hiyo. Hata hivyo haukutaja fidia yoyote utakayotoa kwa familia hiyo iliyosalia bila ya msaada wowote wa kifedha ili kugharamia shughuli za mazishi na gharama za hospitali kwa majeruhi wengine wa ajali hiyo iliyosababishwa na mwanadiplomasia wao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni