Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania alisema jana kuwa uhusiano wa
nchi yake na Rwanda umeharibika kutokana na juhudi zake za kurejesha
amani katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia. Akihutubia wananchi
katika hotuba yake ya kila mwezi, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania
amesema kuwa nchi yake hata hivyo inataka kuendeleza uhusiano wake wa
kihistoria na Rwanda huku ikifanya jitihada za kurejesha amani huko
Kongo. Tanzania inaongoza kikosi kipya cha uingiliaji kati cha Umoja wa
Mataifa huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambako waasi
wa harakati ya Machi 23, kundi ambalo wengi wa wapiganaji wake ni wa
kabila la Watutsi na ambao kwa kiasi kikubwa wanasadikiwa kuwa
wanaungwa mkono na Rwanda, wamekuwa wakiendesha mapigano dhidi ya jeshi
la Kongo na makundi mengine ya waasi mashariki mwa nchi hiyo. Hata hivyo
Rwanda imekanusha tuhuma hizo za kuwaunga mkono waasi wa M23.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni