Jumatano, 19 Juni 2013

usishituke! Ndege za kivita zitatawala anga la Tanzania atakapozuru Obama.

 
 
 
*Azuiwa kutembelea mbuga ya Mikumi 
 *Kisa kubana matumizi, makachero wahaha
 
 

Rais Barrack Obama wa Marekani
ZIARA ya Rais Barack Obama wa Marekani, anayotarajia kuifanya nchini Tanzania imengia doa, baada ya Ikulu ya Marekani, White House, kufuta safari ya kitalii katika Mbunge ya wanyama ya Mikumu. Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na Gazeti la Washington Post juzi, Rais Obama na mkewe, Michelle, hawatakwenda Mikumi kutokana na ufinyu wa bajeti.

Gazeti hilo, likikariri nyaraka za mpango wa kikosi cha makachero wanaomlinda Rais, zilieleza kuwa safari za kitalii, wakati akiwa katika ziara ya Afrika itakayofanyika baadaye mwezi huu, zitahitaji makachero wanaomlinda kuchukua tahadhari kubwa zaidi.

“Safari za kitalii zitahitaji timu maalumu ya udunguaji kubeba bunduki zenye teknolojia ya hali ya juu inayoweza kuwatuliza duma, simba na wanyama wengine iwapo watakuwa tishio,” gazeti hilo limeripoti.
ObamaOdingaSupporter.jpg
Rais Obama ambaye ameamua kukatiza ziara yake ya kitalii Tanzania kwa ajili ya kushughulikia kwanza matatizo ya wananchi wake.
.
army 1.jpg

Magari ya kivita 56 ambayo yatatakiwa kumsindikiza Obama katika safari yake ya kitalii Tanzania


 article-2341276-1A4EBD7F000005DC-211_634x408.jpg
Askari walenga shabaha watakaokuwa wanamlinda na wanyama wakali

navy 1.jpg

Meli ya kivita itakayokuwa ufukweni ikiwa na ndege za kivita na wafanyakazi wa dharura na wauguzi.


Magari 14 aina ya limo ambayo yatakuwa yanatumiwa na Obama katika ziara yake Tanzania

 

Ndege za kivita zitakazotumika kuhakikisha usalama wa angani



Ndege ya mizigo ambayo itasafirisha magari ya kifahari kwa ajili ya safari ya Obama


WASHINGTON –
Ikulu ya White House ya Marekani imekatiza safari ya Rais Obama na mkewe Michelle ya kutembelea mbuga ya wanaya ya mikumi iliyopo Tanzania kutokana na ukata unaoikabili  serikali yake. Imeelezwa katika gazeti la Washington Post jana.Gazeti hilo ambalo lilinukuu mipango ya siri ya safari hiyo imesema kuwa safari ya Obama na mkewe ambayo ilikuwa ifanyike baadaye mwezi huu, ingehitaji majasusi wa kumlinda rais huyo kwa  njia za kipekee zaidi kuhakikisha usalama wake na..... mkewe.
  r

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni