MWIGIZAJI Bongo, Halima Yahaya ‘Davina’ amesema licha ya kuwa amejifungua hivi karibuni mtoto wa tatu lakini mahabati anayopata kwa mumewe, yanamfanya aonekane kama kigori.
Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni jijini Dar, Davina alisema amekuwa akiulizwa na watu wengi siri ya mafaniko yake baada ya kujifungua na kuonekana mrembo hivyo jibu ni mahabati ya mumewe.
“Sina kitu kingine chochote kinachonifanya nipendeze zaidi ya kuridhika na jinsi mume wangu anavyonijali kila siku iendayo kwa Mungu,” alisema Davina.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni