Obama ataka msaada kwa Misri uangaliwe upya

Rais wa Marekani Barack Obama ameziamuru idara zinazohusika nchi humo kuangalia upya msaada unaotolewa na nchi yake kwa serikali ya Misri. Wizara ya Usalama ya marekani imesema katika taarifa iliyotolewa jana kuwa Obama amaetoa agizo hilo kutokana na matukio yaliyotokea nchini Misri wiki iliyopita, lakini haikuzungumzia moja kwa moja mapinduzi ya kijeshi yaliyomuondoa rais Mohamad Mursi madarakani. Wakati huo, afisa moja nchini humo, ambae hakutaka jina lake litajwe, amesema mpango wa marekani kuwasilisha ndege za kivita aina ya F-16 kwa nchi hiyo katika wiki chache zijazo bado uko palepale licha ya agizo la rais.  

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni