Ijumaa, 21 Juni 2013

MWANAJESHI WA JESHI LA ANGA AFARIKI

Mnadhimu mkuu wa jeshi la anga la Nicaragua afariki kwenye ajali ya ndege

(GMT+08:00) 2013-06-21 18:21:08
 
Msemaji wa jeshi la Nicaragua Orlando Palacios amethibitisha kuwa, ajali ya helikopita ya jeshi la nchi hiyo aina ya Mi-17 iliyotokea jana imesababisha vifo vya watu 10 akiwemo mnadhimu mkuu wa jeshi la anga.
Palacios amesema waokoaji wamepata baadhi ya miili ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo katika ziwa Managua, kaskazini mwa mji mkuu Managua. Miili iliyopatikana ni pamoja na maofisa waandamizi 7 wa jeshi la anga, wakiwemo mnadhimu mkuu wa jeshi la anga Manuel Lopez, na mkurugenzi wa ujasusi wa jeshi la anga.
Jeshi la anga limeunda kikundi maalum kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni