Jumatano, 19 Juni 2013

Taliban waua wanajeshi wanne wa Marekani

Kundi la Taliban leo limedai kuhusika na shambulio nchini Afghanistan ambalo limewauwa wanajeshi wanne wa Marekani ikiwa ni saa chache tu baada ya serikali ya Marekani kusema itakuwa na mazungumzo na waasi wa kundi hilo juu ya kukomesha mzozo uliodumu zaidi ya muongo mmoja nchini humo. Shambulio hilo la roketi huko Bagram katika kambi kubwa kabisa ya kijeshi inayoongozwa na Marekani kaskazini mwa Kabul linaonyesha usugu wa waasi hao wa itikadi kali ya Kiislamu ambao mara kwa mara wamekuwa wakifaya mashambulizi katika vituo muhimu. Kabla ya shambulio hilo Rais wa Marekani, Barack Obama, aliyakaribisha mazungumzo na kundi hilo yaliyopangwa kufanyika Qatar akisema ni hatua muhimu.


SOURCE---IDHAA YA KISWAHILI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni