
MWIGIZAJI mahiri Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ Jumatano iliyopita alizua hekaheka mtaani baada ya kutinga kwenye duka moja na watu kumtumbulia macho kwa kumshangaa.

Baadhi ya watu waliokuwa wanapita jirani, walimkodolea macho Lulu huku kila mtu akisema lake. Mtu mmoja ambaye hakutambulika jina, alisikika akisema:
“Ametulia siku hizi, tangu ametoka Segerea amekuwa mtulivu sana.”
Baada ya kuhudumiwa, Lulu alitoka lakini baadaye akagundua kuwa amesahau funguo ya gari, hali iliyomlazimu kurudi dukani.
Aliporudi dukani, aliiona funguo hiyo, akatoka na kwenda kwenye gari alilokuja nalo. Ndani ya gari hilo aina ya Toyota Mark II, alikuwa na mdogo wake ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
sOURCE GLOBAL PUBLISHERS
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni