Alhamisi, 8 Agosti 2013

Refa Mwislamu Senegal asimamisha mechi kufuturu



Nchini Senegal refa Mwislamu amesimamisha mechi ya soka ili kupata fursa ya dakika chache kufuturu na wenzake baada ya saumu ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Ripoti zinasema kuwa mechi kati ya timu za Casa Sport na Yeggo ilianza dakika 30 kabla ya adhana ya Magharibi na hivyo refa Ousseynou Gueye alilazimika kusimamisha mechi hiyo kwa muda mfupi ili aweze kufuturu.
Baada ya mechi, refa huyo alisema anafahamu kuwa kitendo chake kinakiuka kanuni za soka lakini alichukua uamuzi huo kwa mujibu wa mafundisho ya dini yake ya Kiislamu. Amesema baada ya kufuturu kwa tende na maji aliweza kuendelea na kazi yake akiwa na nishati zaidi katika mechi hiyo ya Julai 14 iliyomalizika kwa sare bila mabao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni