Jumamosi, 17 Agosti 2013


Watu 24 wafariki dunia baada ya feri kuzama Uflipino


Watu wasiopungua 24 wameaga dunia na wengine zaidi ya 270 wametoweka baada ya feri ya kuvushia abria kugongana na meli ya mizigo huko katikati mwa Ufilipino. Ajali hiyo ilitokea jana umbali wa kilomita mbili kutoka pwani katika bandari ya Cebu katikati mwa Ufilipino. Feri ya MV Thomas Aquinas iliyokuwa imebeba abiria 870 ilikuwa ikielekea katika bandari ya Cebu ambapo iligongana na meli ya mizigo  na kusababisha ajali hiyo ambapo feri ilizama.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni