Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Maalim Seif Sharif Hamad, ametangaza azma yake ya kuendelea kugombea
urais visiwani humo pamoja na ukatibu mkuu wa Chama chake cha Wananchi
(CUF). Akizungumza wakati wa kutathmini miaka mitatu ya utendaji wa
serikali ya umoja wa kitaifa visiwani Zanzibar hapo jana, Maalim Seif
Sharif Hamad alisitiza kuwa, atastaafu siasa pale atakapoishiwa na nguvu
mwilini, na kwamba licha ya watu fulani kumuona kuwa ni kizingiti kwa
matakwa yao, hataacha nia yake hiyo ya kuwatumikia Wazanzibari. Kuhusu
kugombea tena nafasi yake ya ukatibu mkuu katika uchaguzi wa CUF
utakaofanyika mwakani na urais wa Zanzibar mwaka 2015, Seif alisema kuwa
atatoka tu endapo wanachama wataamua kutomchagua tena. Maalim Seif
alianza kugombea urais wa Zanzibar kwa mara ya kwanza mwaka 1995 baada
mfumo wa vyama vya vingi kurejeshwa rasmi nchini Tanzania lakini ukitoa
uchaguzi uliopita, mara zote amekuwa akilalamika kwamba anapokwa ushindi
na akitangazwa mgombea wa chama tawala cha CCM kuwa mshind
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni