Watu wasiopungua 13 wameuawa na
makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kutokea mlipuko mkubwa wa bomu nje
ya hoteli moja katikati mwa Somalia. Duru za usalama za Somalia
zinaarifu kwamba, mlipuko huo wa bomu umetokea leo nje ya hoteli moja
katika mji wa Baladweyne ulioko katikati mwa nchi hiyo. Aghalabu ya
waliouawa katika mlipuko huo ni wanajeshi. Hoteli hiyo iko jirani na
kambi ya jeshi mjini Baladweyne na inatumiwa zaidi na wanajeshi wa
Ethiopia na wa serikali ya mpito ya Somalia. Licha ya kuwa hadi sasa
hakuna kundi lililotangaza kuhusika na mlipuko huo, lakini vyombo vya
usalama vya Somalia vinaliekezea kidole cha tuhuma kundi la wanamgambo
wa Al-Shabab ambao wamekuwa wakiendesha mapambano dhidi ya vikosi vya
serikali na majeshi ya nchi za Afrika yanayoshirikiana nayo. Hivi
karibuni Umoja wa Afrika ulitangaza kuwa, unapanga mikakati ya kuongeza
idadi ya askari wa kulinda amani nchini Somalia AMISOM, kwa shabaha ya
kupambana na wanamgambo wa kundi la al Shabab.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni