
Boti ya Mali ikizama baada ya kupasuka
en.trend.az
Watu Ishirini wamefariki dunia, wakiwemo watoto 15 , baada ya
boti waliyokuwemo kupasuka usiku wa kuamkia leo kwenye mto Niger karibu
na mji wa Mopti nchini Mali maafisa wamesema na kuongeza kuwa watu 23
hawajulikani walipo na wengine 120 wamenusurika.
Kamanda Dramane Diallo, kutoka timu ya huduma ya uokozi
ameiambia AFP kuwa chanzo cha kupasuka kwa boti hiyo bado hakijafahamika
na kwamba uchunguzi unaendelea.
Afisa mwandamizi wa serikali kamanda Naman Keita, amethibitisha idadi ya watu 20 kupoteza maisha na kuongeza kuwa watoto 15 ni miongoni mwa waliopoteza maisha ambapo zoezi la kutafuta manusura lilisitishwa usiku huo na litaanza tena leo asubuhi.
Kamanda Dramane pia amesema boti hiyo ilijazwa na mizigo kupita kiasi jamboa ambalo huenda likawa miongoni mwa sababu za kupasuka kwa boti hiyo.
Dramane ameongrza kuwa shughuli za uokozi za kikosi cha Mali zimefanyika kwa ushirikiano na wakazi wa mji wa Koubi pamoja na boti zingine zilizokuwa zikipita.
Afisa mwandamizi wa serikali kamanda Naman Keita, amethibitisha idadi ya watu 20 kupoteza maisha na kuongeza kuwa watoto 15 ni miongoni mwa waliopoteza maisha ambapo zoezi la kutafuta manusura lilisitishwa usiku huo na litaanza tena leo asubuhi.
Kamanda Dramane pia amesema boti hiyo ilijazwa na mizigo kupita kiasi jamboa ambalo huenda likawa miongoni mwa sababu za kupasuka kwa boti hiyo.
Dramane ameongrza kuwa shughuli za uokozi za kikosi cha Mali zimefanyika kwa ushirikiano na wakazi wa mji wa Koubi pamoja na boti zingine zilizokuwa zikipita.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni