Ijumaa, 15 Novemba 2013

China italegeza sheria yake inayoruhusu wanandoa kuwa na mtoto mmoja tu kama sera ya upangaji uzazi katika taifa hilo lenye idadi kubwa ya watu ulimwenguni na pia itafutilia mbali sheria yake ya kuwapeleka katika kambi za mateso watuhumiwa wa makosa madogo madogo kama hatua ya kurekebishwa tabia. Hayo yametangazwa leo baada ya viongozi wa chama tawala cha kikomunisti kukutana. Kubadilishwa kwa sera ya kupanga uzazi sasa itaziruhusu familia kuwa na watoto wawili lakini iwapo tu mmoja wa wazazi hao ni mtoto wa pekee kwao. Sera hiyo ya kuwa na mtoto mmoja ilianzishwa katika miaka ya sabini kudhibiti idadi ya watu katika taifa hilo lakini imekuwa ikishutumiwa na mashirika ya kutetea haki za binaadamu kuwa inatekelezwa wakati mwingine kwa njia za kinyama kama kulazimishwa kuavya mimba au kufungwa kizazi. Shirika la habari la serikali, Xinhua, limesema sera hiyo itatekelezwa hatua kwa hatua.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni