Na Jacob Malihoja
Intellectuals na viongozi wakubwa wanapoingia kwenye mkumbo wa kuhisi na kugeuza hisia kuwa ushahidi na kutuhumu wenzao ni aibu!.
===========================
Huu ni udhaifu mkubwa wa kifikra.
Kiongozi, wala Intellectual hawapaswi kutumia taarifa za kuhisi, taarifa za kimajungu kutoa shutuma. Sifa za intellectual na kiongozi makini ni pamoja na kuchambua linalomjia na kujaribu kutafuta vyanzo yakinifu kuhakiki mambo hasa linapokuja suala la shutuma kwa mtu yeyote. Tupo katika kipindi cha vita za kisiasa, sasa kiongozi unasikia jambo tu unakurupuka na kulalama na kutuhumu bila kutafakari kuwa taarifa hizi zaweza kuja kwangu na upepo wa upande gani, huo ni udhaifu uliopitiliza.
Nape Moses
Mnauye, January Makamba, Livingstone Lusinde na wengine wenye mawazo
yafananayo mngemwambia Rais Dr. Jakaya Mrisho Kikwete aivunje TAKUKURU
maana miaka nenda rudi mnalalama haijakamata tukio hata moja wakati
nyinyi mnayajua na mnayaona, basi haina kazi ya kufanya. Au labda
tuwaite nyinyi ni wazembe maana mnaona matukio hampeleki TAKUKURU
yafanyiwe kazi.
Inaonekana nyinyi mna wataalamu wa kuona rushwa na michezo hiyo kuliko TAKUKURU, ama TAKUKURU miaka yote wanaona ila wameshindwa kazi. Ivunjeni .. Wekeni hao watu wenu wanaowaletea hizo taarifa mnazozitumia kushutumu wenzenu .. Maana hao ndio wanaoweza kazi.
Sheria inasema mwananchi ana haki ya kukamata .. Basi nendeni mkakamate nyinyi hayo matukio mnayolalama .. Mana TAKUKURU .. POLISI wameshindwa.. ..
Wenye Hekima wanashindwa kuwaelewa .. Miaka yote vyombo vizito vya kitaifa havija toa taarifa yoyote, havija lalamika .. Havijashuhudia .. Ila nyinyi mna macho zaidi kujua hayo.. Ya kuona hayo .. Hizo taasisi mmeweka za nini .. Vunjeni kitengo cha Usalama wa Taifa, Vunjeni jeshi la polisi, vunjeni TAKUKURU .. Wekeni hao watu wenu wanaowaletea hizo taarifa maana ndio wanaweza kazi kuliko taasisi zote.
Kwa wenye hekima, watafiti na wachambuzi wa mambo kwa kina tunajua hakuna lingine linalowasukuma ni makundi, vita ya urais .. Mnaumizwa na kiwango kikubwa cha kukubalika kwa Edward Lowassa. Hivi mmeangalia maboriti kwenye macho yenu.. hivi ni mangapi mmefanya na mnafanya ..wengine walidiriki hata kuhamasisha kuanzisha chama cha kisiasa na kuchangia uanzishwaji wake nje ya CCM, wengine wamechapisha vitabu na mambo kadha wa kadha zikiwa ni kampeni za chini chini .. mbona maboriti hayo kwenye macho yenu hamyasemi.
Hivi ni nani aambiwe tunakuja kukutembelea akakaa kimya asiandae mapokezi ya wageni wake.. Hivi nyinyi kwenu mnapokuwa na wageni hamuandai kuwapokea? Au mtu anayetazamiwa kugombea urais anatakiwa kuwa kama ROBOT? Asicheke na watu, asishiriki na watu, asipokee wageni .. Wageni wakija waje kivyao .. Pengine wachungulie tu madirishani waondoke.
Mngewawekea kanuni ya kukataa wageni pia ili wasionekane wanafanya kampeni .. Mbona hamkuweka .. Nani ana tatizio hapo ..acheni kulalama .. Kwa tabia hiyo mnatufunulia kuwa ninyi ndio Wasaliti wakubwa wa CCM, Nyinyi ndio mnataka kukigawa chama .. nyinyi mko tayari CCM iwe Chama Cha upinzani lakini Lowassa asiende ikulu .. Wasaliti wakubwa wa Watanzania, Mnaitukana Serikali kwa Vyombo vyake kushindwa kazi na kujionesha nyinyi ndio mnaona maovu .. Wasaliti wakubwa wa umoja na mshikamano wa Chama Cha Mapinduzi. Mnawatukana mamilioni ya watanzania, wenye mapenzi kwa Lowassa eti wanalipwa kufanya hivyo,huo ni usaliti kwa watu wenu .. na mwisho mnamtukana Rais Dr. Jakaya Kikwete aliyehamasisha watu kama wanamwona mtu anaweza wakamshawishi.
Acheni wananchi, Acheni wana CCM waamue.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki CCM
Mungu Wabariki viongozi wa CCM na uwajaze hekima waache tabia ya Kugeuza hisia kuwa Ushahidi na kutengeneza tuhuma.
source Jacob Malihoja facebook page
Inaonekana nyinyi mna wataalamu wa kuona rushwa na michezo hiyo kuliko TAKUKURU, ama TAKUKURU miaka yote wanaona ila wameshindwa kazi. Ivunjeni .. Wekeni hao watu wenu wanaowaletea hizo taarifa mnazozitumia kushutumu wenzenu .. Maana hao ndio wanaoweza kazi.
Sheria inasema mwananchi ana haki ya kukamata .. Basi nendeni mkakamate nyinyi hayo matukio mnayolalama .. Mana TAKUKURU .. POLISI wameshindwa.. ..
Wenye Hekima wanashindwa kuwaelewa .. Miaka yote vyombo vizito vya kitaifa havija toa taarifa yoyote, havija lalamika .. Havijashuhudia .. Ila nyinyi mna macho zaidi kujua hayo.. Ya kuona hayo .. Hizo taasisi mmeweka za nini .. Vunjeni kitengo cha Usalama wa Taifa, Vunjeni jeshi la polisi, vunjeni TAKUKURU .. Wekeni hao watu wenu wanaowaletea hizo taarifa maana ndio wanaweza kazi kuliko taasisi zote.
Kwa wenye hekima, watafiti na wachambuzi wa mambo kwa kina tunajua hakuna lingine linalowasukuma ni makundi, vita ya urais .. Mnaumizwa na kiwango kikubwa cha kukubalika kwa Edward Lowassa. Hivi mmeangalia maboriti kwenye macho yenu.. hivi ni mangapi mmefanya na mnafanya ..wengine walidiriki hata kuhamasisha kuanzisha chama cha kisiasa na kuchangia uanzishwaji wake nje ya CCM, wengine wamechapisha vitabu na mambo kadha wa kadha zikiwa ni kampeni za chini chini .. mbona maboriti hayo kwenye macho yenu hamyasemi.
Hivi ni nani aambiwe tunakuja kukutembelea akakaa kimya asiandae mapokezi ya wageni wake.. Hivi nyinyi kwenu mnapokuwa na wageni hamuandai kuwapokea? Au mtu anayetazamiwa kugombea urais anatakiwa kuwa kama ROBOT? Asicheke na watu, asishiriki na watu, asipokee wageni .. Wageni wakija waje kivyao .. Pengine wachungulie tu madirishani waondoke.
Mngewawekea kanuni ya kukataa wageni pia ili wasionekane wanafanya kampeni .. Mbona hamkuweka .. Nani ana tatizio hapo ..acheni kulalama .. Kwa tabia hiyo mnatufunulia kuwa ninyi ndio Wasaliti wakubwa wa CCM, Nyinyi ndio mnataka kukigawa chama .. nyinyi mko tayari CCM iwe Chama Cha upinzani lakini Lowassa asiende ikulu .. Wasaliti wakubwa wa Watanzania, Mnaitukana Serikali kwa Vyombo vyake kushindwa kazi na kujionesha nyinyi ndio mnaona maovu .. Wasaliti wakubwa wa umoja na mshikamano wa Chama Cha Mapinduzi. Mnawatukana mamilioni ya watanzania, wenye mapenzi kwa Lowassa eti wanalipwa kufanya hivyo,huo ni usaliti kwa watu wenu .. na mwisho mnamtukana Rais Dr. Jakaya Kikwete aliyehamasisha watu kama wanamwona mtu anaweza wakamshawishi.
Acheni wananchi, Acheni wana CCM waamue.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki CCM
Mungu Wabariki viongozi wa CCM na uwajaze hekima waache tabia ya Kugeuza hisia kuwa Ushahidi na kutengeneza tuhuma.
source Jacob Malihoja facebook page