......One of the cardinal principles of Economics is Opportunity Cost. Do the
fast thing first, and those which can wait let them wait.....
Hebu tujaribu kufanya hesabu ndogo za kugawanya na kuzidisha za darasa la tano. Ni hivi, wabunge wawili walioteuliwa watalipwa mishahara ya miezi mitano bure maana hatutegemei jipya watakalolifanya huko bungeni. Mshahara kwa mbunge mmoja ni Mil.11 mara miezi mitano watakayofanya kazi ni jumla ya Sh.Mil 55 kwa kila mmoja. Kwa wote wawili ni Mil.110.
Wabunge hawa walioteuliwa leo watalipwa kiinua mgongo kwa viwango vya wabunge wa kawaida Sh.Mil.90 kila mmoja ifikapo tar.31 mwezi July mwaka huu. Kwa wote wawili ni Mil.180.
Taarifa ya Ikulu inasema uteuzi wao unaanza tarehe 20, hivyo basi kuanzia tar.21 wataanza kulipwa posho za vikao vya bunge kwa siku 10 zilizobakia kwenye bunge hili linaloendelea. Posho ya siku moja ni Sh.330,000/= kwa siku kumi ni Mil.3 na laki 3.
Kwenye bunge la bajeti Watalipwa posho ya 330,000/= kwa siku. Bunge hilo litatumia jumla ya siku 60. Hivyo mbunge mmoja atalipwa Mil.19 na laki 8, kwa muda wote wa bunge la bajeti. Kwa wote wawili watalipwa mil.39 na laki 6.
Wabunge hawa "watakopeshwa" magari ya kifahari ya kutembelea. Yani kama walikua wakitumia usafiri wa umma, kuanzia tar.20 March wameambiwa stop. Watapanda Mashangingi yanayokadiriwa kugharimu Mil.120 kwa moja, kwa wote wawili ni Mil.240.
Kwa ujumla makadirio ya gharama zote za wabunge hawa wawili kwa miezi mitano tu watakayofanya kazi watatumia jumla ya Shilingi Milioni 573 na laki 2.
Pesa hizi zinatosha kulipia mikopo ya elimu ya juu kwa semester moja kwa wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza Chuo kikuu cha St.Augustine, au Chuo Kikuu Dodoma kwa wanafunzi wanaosoma Social Science.
Pia pesa hizi zingeweza kujenga maabara za kisasa katika shule 12 Tanzania. Zingeweza kulipa mishahara ya waalimu (daraja la pili) 1,432 wa shule mbalimbali za sekondari nchini. Pia fedha hizi zingeweza kutolewa kama mkopo kwa vijana wanaohitimu vyuo vya Elimu ya juu nchini na kukosa ajira. Jumla ya vijana 573 wangenufaika kwa mkopo wa Mil.1 kila mmoja.
Lakini cha ajabu pesa zote hizi zitatumiwa na wabunge wawili tu tena kwa kipindi cha miezi mitano tu, with no expectation of return. Hatutegemei wabunge hawa watafanya lolote jipya huko bungeni litakalogharimu hizo Mil.573 watakazotumia.
Kwa lugha rahisi ni kuwa hatutegemei output ya wabunge hawa izidi input. Hakuna mbunge yeyote atakayeweza kutoa hoja zitakazo-value hizo Mil.573 watakazotumia, hata wakisaidiwa na huyo aliyewateua.
Sasa nimejiuliza, hivi katika mazingira haya ambayo hatuna rasilimali za kutosha kulinganisha na mahitaji tuliyonayo, je kulikua na ulazima wowote wa kuteua wabunge hao?
Tunahitaji pesa za kujenga maabara, kujenga shule, kulipia wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu mikopo, kulipa mishahara, kununua madawa etc. Lakini tumeacha vyote hivyo tumetoa kipaumbele kwa wabunge tena wa kuteuliwa.
Tafakri......
Hebu tujaribu kufanya hesabu ndogo za kugawanya na kuzidisha za darasa la tano. Ni hivi, wabunge wawili walioteuliwa watalipwa mishahara ya miezi mitano bure maana hatutegemei jipya watakalolifanya huko bungeni. Mshahara kwa mbunge mmoja ni Mil.11 mara miezi mitano watakayofanya kazi ni jumla ya Sh.Mil 55 kwa kila mmoja. Kwa wote wawili ni Mil.110.
Wabunge hawa walioteuliwa leo watalipwa kiinua mgongo kwa viwango vya wabunge wa kawaida Sh.Mil.90 kila mmoja ifikapo tar.31 mwezi July mwaka huu. Kwa wote wawili ni Mil.180.
Taarifa ya Ikulu inasema uteuzi wao unaanza tarehe 20, hivyo basi kuanzia tar.21 wataanza kulipwa posho za vikao vya bunge kwa siku 10 zilizobakia kwenye bunge hili linaloendelea. Posho ya siku moja ni Sh.330,000/= kwa siku kumi ni Mil.3 na laki 3.
Kwenye bunge la bajeti Watalipwa posho ya 330,000/= kwa siku. Bunge hilo litatumia jumla ya siku 60. Hivyo mbunge mmoja atalipwa Mil.19 na laki 8, kwa muda wote wa bunge la bajeti. Kwa wote wawili watalipwa mil.39 na laki 6.
Wabunge hawa "watakopeshwa" magari ya kifahari ya kutembelea. Yani kama walikua wakitumia usafiri wa umma, kuanzia tar.20 March wameambiwa stop. Watapanda Mashangingi yanayokadiriwa kugharimu Mil.120 kwa moja, kwa wote wawili ni Mil.240.
Kwa ujumla makadirio ya gharama zote za wabunge hawa wawili kwa miezi mitano tu watakayofanya kazi watatumia jumla ya Shilingi Milioni 573 na laki 2.
Pesa hizi zinatosha kulipia mikopo ya elimu ya juu kwa semester moja kwa wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza Chuo kikuu cha St.Augustine, au Chuo Kikuu Dodoma kwa wanafunzi wanaosoma Social Science.
Pia pesa hizi zingeweza kujenga maabara za kisasa katika shule 12 Tanzania. Zingeweza kulipa mishahara ya waalimu (daraja la pili) 1,432 wa shule mbalimbali za sekondari nchini. Pia fedha hizi zingeweza kutolewa kama mkopo kwa vijana wanaohitimu vyuo vya Elimu ya juu nchini na kukosa ajira. Jumla ya vijana 573 wangenufaika kwa mkopo wa Mil.1 kila mmoja.
Lakini cha ajabu pesa zote hizi zitatumiwa na wabunge wawili tu tena kwa kipindi cha miezi mitano tu, with no expectation of return. Hatutegemei wabunge hawa watafanya lolote jipya huko bungeni litakalogharimu hizo Mil.573 watakazotumia.
Kwa lugha rahisi ni kuwa hatutegemei output ya wabunge hawa izidi input. Hakuna mbunge yeyote atakayeweza kutoa hoja zitakazo-value hizo Mil.573 watakazotumia, hata wakisaidiwa na huyo aliyewateua.
Sasa nimejiuliza, hivi katika mazingira haya ambayo hatuna rasilimali za kutosha kulinganisha na mahitaji tuliyonayo, je kulikua na ulazima wowote wa kuteua wabunge hao?
Tunahitaji pesa za kujenga maabara, kujenga shule, kulipia wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu mikopo, kulipa mishahara, kununua madawa etc. Lakini tumeacha vyote hivyo tumetoa kipaumbele kwa wabunge tena wa kuteuliwa.
Tafakri......
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni