Jumatano, 26 Juni 2013
Afya ya mandera kutoathiri ziara ya Obama
Zuma amesema yeye na makamu wa rais wa chama cha Africa National Congress, ANC, Cyril Ramaphosa walimtembelea Mandela usiku wa kuamkia leo. Lakini amekataa kutoa maelezo zaidi kuhusu afya ya Mandela, zaidi ya kusema kuwa yuko katika hali mbaya sana. Rais wa Marekani Barack Obama anatarajiwa kufanya ziara nchini Afrika Kusini wiki hii, lakini Zuma amesema kuwa kudorora kwa afya ya Mandela hakutaathiri ziara hiyo.
Kudorora kwa afya ya Mandela wikendi hii, ikiwa ni wiki mbili tangu alipolazwa akiwa katika hali mbaya lakini imara, kumeibadili hali kutoka kwenye kumuombea kupona haraka hadi kwenye kuanza maandalizi ya kumuaga. "Kama ni wakati wa yeye kuondoka, anaweza kuondoka, namuombea kwa Mungu ampokee vyema," alisema Petunia Mafuyeka, ambaye ni Nesi wakati akielekea kazini mjini Johannesburg.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni