Rais wa Marekani Barack Obama anaanza ziara yake ya pili barani Afrika
wiki hii katika nchi tatu,Senegal,Afrika Kusini na Tanzania.
Kwa mara nyingine tena Obama ambaye babake ni mzaliwa wa Kenya hataizuru
nchi hiyo na badala yake amechagua nchi jirani ya Tanzania,suala hili
limezua mjadala mkali nchini Kenya hasa ikizingatiwa naye Rais Uhuru
Kenyatta wiki hii pia anaanza ziara barani Asia na kuzua hoja ya je ni
wakati wa Kenya kuelekeza macho yake Mashariki. Caro Robi amezungumza na
mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Kenya Herman Manyora na kwanza
alimuuliza nini mtazamo wake kuhusiana na suala hili? Kusikiliza
mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni