HAWAONI YALIYOTOKEA KWA CASILLAS & MOURINHO
Ni ukweli usiofichika kwamba, kipa Iker Casillas ndiye kila kitu kati ya wachezaji wa Real Madrid na hata timu ya taifa ya Hispania. Kocha Jose Mourinho muda mfupi baada ya kutua kuifundisha klabu hiyo alitaka kufuta hali hiyo kwa Casillas.
Mourinho alitaka yeye kuwa mtu muhimu katika timu kuliko Casillas, akamtengezea mazingira kipa huyo ya kuonekana hafai na kuanza kumuweka benchi bila sababu ya msingi.
Hata hivyo, Madrid ni miongoni mwa klabu zinazothamini mchango wa wakongwe kama Casillas ambao wanaweza kuisaidia timu ndani na nje ya uwanja. Ikaamua kuachana na Mourinho ili ibaki na Casillas.
Ndiyo maana Chelsea leo hii ina John Terry, Liverpool yupo Steven Gerrard, Man United wanaye Giggs, na hata Yanga wanaye Shadrack Nsajigwa. Sasa iweje Simba imtimue Kaseja?
Umefika wakati sasa siasa na chuki zisizo na maana ziondoke katika mazingira ya soka letu ili tuweze kufikia mafanikio.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni