Na Gladness Mallya
HATIMAYE
wale wapenzi waliong’aa hivi karibuni, mwigizaji Tamrina Mohamed Poshi
‘Amanda’ na Mbongo Fleva, Joseph Rushahu ‘Bwana Misosi’ wanadaiwa
kumwagana rasmi, Ijumaa limetonywa.
Tamrina Poshi ‘Amanda’ akiwa na mpenzi wake wanayedaiwa kumwagana naye, Emmannuel Rushau ‘Bwana Misosi’.
Habari kutoka chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa wapenzi hao,
zilieleza kuwa Amanda na Bwana Misosi walishamwagana kimyakimya ikiwa ni
baada ya kushindwa kuelewana kitabia.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, mwanahabari wetu alimtafuta Amanda ili aelezee ukweli kuhusu habari hizo ambapo alikiri kuwa ni kweli wameshaachana na hii ni baada ya kushindwana kitabia.
“Mimi na (Bwana) Misosi tumeachana muda mrefu tangu mwezi wa pili baada ya kushindwana na katika uhusiano wa kimapenzi, nimejifunza kuwa wanaume siyo watu wa kuwaamini asilimia mia moja kwani baadaye unaweza kujuta,” alisema Amanda.
Kwa upande wake Bwana Misosi hakuweza kujibu moja kwa moja swali aliloulizwa bali alianza kwa kujikanyagakanyaga
“Kwanza niko safarini, je, ni nani aliyekuambia hizo habari….hebu ngoja nimpigie huyo Amanda nimuulize nani aliyetoa siri hiyo,” alisema Misosi.

Baada ya kuzinyaka habari hizo, mwanahabari wetu alimtafuta Amanda ili aelezee ukweli kuhusu habari hizo ambapo alikiri kuwa ni kweli wameshaachana na hii ni baada ya kushindwana kitabia.
“Mimi na (Bwana) Misosi tumeachana muda mrefu tangu mwezi wa pili baada ya kushindwana na katika uhusiano wa kimapenzi, nimejifunza kuwa wanaume siyo watu wa kuwaamini asilimia mia moja kwani baadaye unaweza kujuta,” alisema Amanda.
Kwa upande wake Bwana Misosi hakuweza kujibu moja kwa moja swali aliloulizwa bali alianza kwa kujikanyagakanyaga
“Kwanza niko safarini, je, ni nani aliyekuambia hizo habari….hebu ngoja nimpigie huyo Amanda nimuulize nani aliyetoa siri hiyo,” alisema Misosi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni