Jumapili, 28 Julai 2013

MSICHANA ANYONGWA NA MPENZI WAKE

 Bagamoyo Pwani
MSICHANA Rehema Athumani Mpendae, ameuawa kikatili kwa kunyongwa na mtu anayedhaniwa kuwa ni mpenzi wake huku chanzo cha kufanyiwa unyama huo kikiwa hakijulikani.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa watu waliopanga katika nyumba moja na marehemu, wamekadiria kuwa Rehema alinyongwa saa 12 jioni kwenye nyumba aliyokuwa akiishi katika eneo la Majani Mapana wilayani hapo.
Alisema baada ya polisi kupata taarifa walifika katika eneo la tukio na kukuta msichana huyo akiwa amedhalilishwa na kuuawa kinyama kisha wakamuita.
 “Baada ya kufika kwenye nyumba hiyo nikatakiwa na polisi kuingia ndani ili kujua kama kuna mtu katika chumba cha marehemu,” alisema Matata.
Aliongeza kuwa mara baada ya kuingia ndani aliukuta mwili wa binti huyo ukiwa umelazwa kitandani bila ya nguo huku ukiwa umefunikwa, mdomoni akiwa amezibwa kwa kanga.
Mmoja wa wapangaji wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Fauzia Abdallah (20), alisema kuwa mara ya mwisho kumuona Rehema ilikuwa ni Ijumaa jioni ya Julai 19, mwaka huu.
“Siku hiyo ilipofika  jioni nilimsikia akizungumza kwa simu huku akimtaka mtu ambaye inaonekana alikuwa mpenzi wake na hakuwa mbali na hapa akimwambia amsubiri ili waonane.
“Alitoka ndani na baada ya muda nilimsikia akiingia na mtu ambaye alikuwa na sauti ya kiume lakini kwa sababu nilikuwa ndani kwangu nikiangalia TV, sikuweza kumuona au kumfahamu,” alisema Fauzia.
Alifafanua kuwa kama saa 12 hivi jioni alisikia wakiwa wanabishana lakini hakuweza kujua walibishania kitu gani na baadaye kukawa kimya na hawakuonana tena hadi aliposikia kesho yake kuwa ameuawa kikatili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni