Jumatatu, 8 Julai 2013

Ghasia za Misri zalaaniwa vikali

Idadi ya waliouawa Misri imefikia 51 na waliojeruhiwa ni zaidi ya 400.Ujerumani imetaka kufanywe uchunguzi huru kuhusiana na mauaji hayo ya waandamanaji waliokuwa wanamuunga mkono rais aliyeng'olewa madarakani nchini Misri, Muhammed Mursi, leo alfajiri na jeshi la nchi hiyo. Wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani imetoa taarifa leo mjini Berlin ikielezea kushitushwa kwake na mauaji hayo na kuzitaka pande zote husika kujizuia kumwaga damu ikiongeza inahofia ghasia hizo zinazidi. Kundi la Udugu wa Kiislamu limesema wafuasi wake wameuawa na vikosi vya usalama walipokuwa wakisali nje ya makao makuu ya jeshi mjini Cairo.Rais wa muda wa Misri, Adly Mansour, pia ameitisha uchunguzi rasmi kuhusiana na mauaji hayo ya leo. Msemaji wa serikali ametoa taarifa kuwa mipango ya kuunda serikali ya muungano itaendelea licha ya matukio hayo ya leo. Qatar nayo imeyalaani mauaji hayo na kutaka kusitishwa kwa ghasia mara moja, huku Umoja wa Ulaya ukisema unatathimini ahadi zake za kuipa nchi hiyo misaada ya mabilioni ya euro kutokana hali tete iliyopo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni