Jumapili, 28 Julai 2013

Idadi ya vifo kutokana na mapambano ya ijumaa kati ya wafuasi na wapinzani wa Morsi yaongezeka na kufikia 139 nchini Misri


Idadi ya vifo vilivyotokana na mapambano ya ijumaa kati ya wafuasi na wapinzani wa rais aliyeondolewa madarakani wa Misri Mohammed Morsi imeongezeka na kufikia 139. Kwa mujibu wa taarifa ya chama cha Muslim Brotherhood, watu 120 wameuawa na wengine zaidi ya 4,500 kujeruhiwa katika mapambano kati ya wafuasi wa Morsi na maafisa wa usalama karibu na msikiti wa Rabaa al-Adaweya mjini Nasr. Muslim Brotherhood imesema wengi wa wahanga hao walikuwa na majeraha ya risasi kichwani, shingoni na kifuani ambayo walipata kutoka kwa walenga shabaha.Vikosi vya polisi vinadaiwa kufyatua risasi kutawanya umati wa wafuasi wa Morsi waliokuwa wamekusanyika katika kambi ya kijeshi katika mtaa wa Naser. Ijumaa, mapambano makali kati ya wafuasi na wapinzani wa Mohammed Morsi yalitokea katika mkoa wa Alexandria na mikoa mingine nchini Misri na kusababisha vifo vya watu 19.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni