Ijumaa, 19 Julai 2013

Magaidi wa Syria waendelea kuuana


Hitilafu na mizozo baina ya makundi ya kigaidi nchini Syria imeshadidi zaidi na waasi hao wameendelea kupigana na kuuana wenyewe kwa wenyewe. Taarifa nchini Syria zinasema kuwa, mapigano hayo yaliyojiri baina ya magaidi wa Jeshi Huru la Syria na Jabhat an-Nasra yamepelekea makumi ya magaidi wa pande mbili kuuawa. Mapigano hayo yanaripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali ya mji wa Idlib ulioko kaskazini magharibi mwa Syria. Hitilafu hizo ambazo katika siku za hivi karibuni zimeshadidi mno chanzo chake kinatajwa kuwa ni juhudi zao za kuwania madaraka na uongozi wa kusimamia makundi yote ya magaidi nchini humo. Hivi karibuni Muadh al Khatib mkuu aliyejiuzulu wa muungano wa wapinzani wa Syria, alikiri kuongezeka mpasuko kati ya wapinzani na kusema kuwa, baadhi yao hawakubaliani na mapendekezo ya muungano huo bali wanachokipigania wao ni madaraka na maslahi yao binafsi. Wakati huo huo, magaidi 120 wa Syria wameuawa katika maeneo mbalimbali ya kaskazini mwa nchi hiyo kufuatia mashambulio ya jeshi la nchi hiyo katika ngome za magaidi hao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni