Jumapili, 28 Julai 2013

Mzee Small anena mazito

 
 

  • Jambo baya zaidi kwake ni kuwa hana vyanzo vya mapato vya kueleweka.
  • Anaendelea kusimulia kwamba  wakati anaugua amekumbwa na mkasa wa binti yake (jina linahifadhiwa) kukatiza masomo kutokana na ujauzito.

WIKI iliyopita tulianza kuona namba mwigizaji, msanii wa vichekesho ambaye pia ni mcheza ngoma za makabila mbalimbali wa Tanzania, Small Wangamba ‘Mzee Small’ anavyosimulia mateso yake ya sasa yanayotokana na maradhi ya kiharusi. Bado hajapata matibabu ya maana kutokana na sababu mbalimbali kubwa ikiwa kukosa uwezo kifedha, endelea…
Mzee Samal anasema alihangaika maeneo tofauti kupata tiba na kuna wakati shabiki wake mmoja aliwekeza fedha katika zahanati moja (jina halikumbuki) iliyopo eneo la Kariakoo ambao alikuwa anapata huduma ya kuchuliwa misuli.
“Huyo mtu alisikia naumwa akatafuta namba zangu za simu kisha akanipigia na kunielekeza sehemu ya kwenda kuchuliwa kwani nae aliwahi kukumbwa na tatizo kama hilo la kupooza mkono, lakini alipata nafuu kidogo,” anasema.
Small anasema tiba hiyo ya kuchuliwa viungo ilimpa nafuu kiasi lakini haikumuwezesha kurejea hali ya kawaida na siku za karibuni mambo yamebadilika. Hivi sasa sehemu ya mkono inapoungana na bega inaachana hali ambayo anasema inazidi kumchanganya.
Hali yake kiuchumi
“Mkono unakuwa kama unatengana na bega na mbaya zaidi nazidi kuishiwa nguvu na sina uwezo walau wa kujikokota na kutembea,” anasema na kuongeza kuwa hivi sasa hawezi kufanya shughuli yoyote zaidi ya kula na kulala.
Jambo baya zaidi kwake ni kuwa hana vyanzo vya mapato vya kueleweka.
“Pesa pekee ambazo zinanisaidia kidogo ni za kuuza maji, haponndiyo napata fedha ya kula na mke wangu Fatma Binti Saidi,” anasema.
Anaendelea kusimulia kwamba  wakati anaugua amekumbwa na mkasa wa binti yake (jina linahifadhiwa) kukatiza masomo kutokana na ujauzito.
Ilikuwa mwaka jana wakati binti hiyo akiwa Kidato cha Tatu.
“Watu wamemtia mimba mwanangu wa kike ambaye alikuwa ni wa tatu, lakini bahati nzuri aliyefanya hivyo ameamua kumuoa, basi sasa nitafanya nini na mimi hali yangu kama unavyoiona?” Anasema na kuongeza kuwa hata hivyo hajakata tamaa.


source mwanasport

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni