Jumapili, 28 Julai 2013

Wafungwa 1,000 watoroka jela Benghazi, Libya


Wafungwa zaidi ya 1,000 wametoroka jela karibu na mji wa Benghazi   Mashariki mwa Libya huku waandamanaji wakiendelea kuvamia ofisi za vyama vya kisiasa nchini humo.
Maafisa wa usalama wanasema wafungwa hao walitoroka Jela ya al Kweifiya siku ya Jumamosi. Imedaiwa kuwa waliotoroka ni pamoja na raia kadhaa wa kigeni kutoka nchi za Afrika waliohusishwa na utawala uliotimuliwa madarakani wa Muammar Gaddafi.
Waziri Mkuu wa Libya Ali Zeidan amethibitisha kutokea tukio hilo na kusema wakaazi wa eneo hilo ndio waliowasaidia wafungwa kutoroka kwa sababu hawataki jela karibu na nyumba zao.
Hadi sasa wafungwa 18 waliotoroka wamekamatwa huku baadhi wakirejea wenyewe gerezani. Katika siku za hivi karibuni kumeibuka maandamano makubwa nchini Libya kufuatia mauaji ya mwanaharakati ambaye alikuwa mkosoaji wa Harakati ya Ikwanul Muslimin. Ofisi kadhaa za harakati hiyo zimeteketezwa moto mjini Benghazi na katika miji mingine ya Libya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni