Jumapili, 28 Julai 2013

Wafungwa 1200 watoroka kutoka gereza la Benghazi nchini Libya


Waziri mkuu wa serikali ya mpito ya Libya Ali Zaidan amesema wafungwa 1200 wametoroka kutoka gereza la Benghazi nchini Libya.
Bw. Zeidan amesema gereza hilo lilishambuliwa na wakazi wa huko ambao hawapendi kuishi karibu na gereza. Kikosi maalum ambacho kina uwezo wa kudhibiti hali ya huko, kilishindwa kuwazuia wakazi walipokuwa wakifungua mlango wa gereza hilo baada ya kupewa amri ya kutowafyatulia risasi wakazi hao. Bw. Zeidan amesema wafungwa waliotoroka watasakwa kote nchini humo, na vituo vya ukaguzi mpakani vitatumiwa orodha ya majina ya wafungwa hao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni