Iran yatengeneza ndege ya kisasa isiyo na rubani
Wataalamu wa Iran wanaunda ndege ya kisasa kabisa ya kivita isiyo ya rubani na yenye uwezo wa kupiga picha za matukio mbali. Kiongozi anayesimamia zoezi hilo Hassan Akbari amesema kuwa, ndege hiyo ina sifa za kipekee katika kutekeleza mashambulizi ya hali ya juu katika mazingira ya kivita. Aidha katika sifa zake nyingine ni pamoja na kuwa na uwezo wa kuzalisha umeme kwa ajili ya kuhifadhi muundo wake na hivyo kuiepusha na hatari tarajiwa. Ameongeza kuwa mbawa za ndege hiyo zina urefu wa sentimita 170 na hivyo kuifanya iweze kuhimili uzito wa ndege na kuwa na uwezo mkubwa wa kuruka. Kwa upande mwingine ndege hiyo, ina uwezo wa kuchukua picha kwa umbali na kisha kuzisajili na kuainisha maeneo ya vita.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni