Jumatatu, 5 Agosti 2013

Mkuu wa zamani wa jeshi Uturuki afungwa maisha jela


Mahakama Kuu nchini Uturuki imemhukumu mkuu wa zamani wa jeshi la nchi hiyo kifungo cha maisha jela baada ya kumpata na makosa ya kushirikiana na wanajeshi waliopanga kuipindua serikali mwongo mmoja uliopita. Ilker Basbug anadaiwa kushirikiana na zaidi ya wanajeshi 1000 kupanga mapinduzi ya kijeshi. Polisi wamelazimika kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa Basbug nje ya mahakama hiyo magharibi mwa mji wa Istanbul. Watu wengine 21 wamefutiwa mashtaka kwenye kesi hiyo huku wengine wakihukumiwa vifungo vya kati ya miaka 12 hadi 20 jela. Wachambuzi wengi wanasema kuwa, Waziri Mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan ametumia kesi hiyo kuwaandama na kuwanyamazisha wapinzani na wakosoaji wa chama chake cha AKP.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni