Wananchi wanaomuunga mkono Muhammad Musri rais aliyepinduliwa wa
Misri kwa mara nyingine wamepanga kuandamana hii leo katika mji mkuu wa
nchi hiyo Cairo, huku harakati ya Ikhwanul Muslimin ikitoa wito wa
kujitokeza kwa wingi wananchi kwenye maandamano hayo. Taarifa
iliyotolewa na 'Muungano wa Kupinga Mapinduzi ya Kijeshi' imesema kuwa,
maandamano kadhaa yamepangwa kufanyika leo katika maeneo mbalimbali ya
Cairo katika kuendeleza kupinga watawala wa kijeshi nchini Misri.
Hayo yanajiri katika hali ambayo Baraza la Mawaziri la Misri linapanga kujadili mgogoro wa nchi hiyo huku Rais Adly Mansour wa serikali ya mpito akitoa pendekezo la kupigwa marufuku Harakati ya Ikhwanul Muslimin ya nchi hiyo.
Hayo yanajiri katika hali ambayo Baraza la Mawaziri la Misri linapanga kujadili mgogoro wa nchi hiyo huku Rais Adly Mansour wa serikali ya mpito akitoa pendekezo la kupigwa marufuku Harakati ya Ikhwanul Muslimin ya nchi hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni