Jumatano, 30 Oktoba 2013

Chelsea yaifunga Arsenal mabao 2 kwa 0 na kufuzu robo fainali ya michuano ya Capital One

Klabu ya soka ya Chelsea imefuzu katika hatua ya robo fainali ya michuano ya kuwania taji la Capital One nchini Uingereza baada ya kuifunga Arsenal mabao 2 kwa 0 Jumanne usiku.

Mchuano huo ulichezwa katika uwanja wa nyumbani wa Arsenal wa Emirates, huku Juan Mata akiifungia Chelsea bao lake la kwanza msimu huu katika kipindi cha pili cha mchuano na kuihakikishia timu yake ushindi baada ya bao la kwanza kutiwa kimyani na Cesar Azpilicueta katika kipindi cha kwanza.
Wachambuzi wa soka wanasema juhudi za wachezaji wa kiungo cha Kati wa Chelsea Michael Essien na John Obi Mikel kumiliki mpira katika eneo hilo lilisadia sana vijana wa Kocha Jose Mourinho kupata ushindi huo wa kuridhisha.
Mchuano huo wa Jumanne usiku ni wa pili kwa Arsenal kufungwa nyumbani baada ya kushindwa kutamba katika uwanja wao mwezi Februari mwaka huu, na kushindwa kwao kumetamatisha ndoto yao ya kunyakua taji hilo la Capital One ambalo wamekuwa wakilisaka kwa miaka minane sasa.
Huu ulikuwa mchuano wa kwanza wa kwa kocha Mourinho kucheza dhidi ya mwenzake Arsene Wenger tangu mwaka 2007.
Mabadiliko ya wachezaji nane yaliyofanywa na Wenger katika mchuano huo yanaelezwa na wachambuzi wa soka kuwa chanzo cha vijana wake kufungwa.
Mbali na mchuano huo, Birmingahm City walitoka sare ya kufungana mabao 4 kwa 4 na Stoke City, na baadaye Stoke City ikafanikiwa kufuzu kwa kushinda Birmingahm City kwa mikwaju ya penalti 4 kwa 2.
West Ham ilifuzu baada ya kuifunga Burnley mabao 2 kwa 0, Leicester City ikaishinda Fulhma mabao 4 kwa 3.
Manchester United nayo iliigaragaza Norwich City mabao 4 kwa 0.
Siku ya Jumatano Newcastle itamenyana na Manchester City, Tottenham Hotspurs nayo ichuane na Hull City.
Wanajeshi wa DRC wiki hii wamefanikiwa kukomboa maeneo mengine kutoka kwa M23
Wanajeshi wa DRC wamefanikiwa kuwatimua waasi wa M23 kutoka katika ngome yao kuu katika eneo la Bunagana.
Wanajeshi hao wamekomboa mji wa Bunagana kufuatia makabiliano makali adhuhuri ya leo ambapo baadhi ya waasi walilazimika kuimbilia msituni huku baadhi wakidai waliingia Uganda baada ya kuvalia mavazi ya kiraia.
Msemaji wa serikali alisema kuwa mji wa Bunagana ulio katika mpaka wa Uganda na DRC, sasa uko chini ya wanajeshi wa serikali.
Wenyeji wa mji huo walithibitishia BBC kuwa mji huo ulikombolewa na kuwa waasi wamekuwa wakitoroka mapambano makali dhidi yao.
Hatua hii ya wanajeshi ni sehemu ya ushindi mkubwa ambao wanajeshi wamekuwa wakiupata dhidi ya waasi hao wa M23 walianza harakati zao dhidi ya serikali ya Congo mwaka jana wakidaiwa kusaidiwa na serikali ya Rwanda.
Mnamo siku ya Jumatatu mjumbe maalum wa M23 hawana tena nguvu za kijeshi kwani sio tesho tena.,
Umoja wa Mataifa umesema kuwa wakimbizi elfu tano wamelazimika kutoroka Bunagana na kuingia Uganda kwa usalama wao.

Raia wanne wa Ufaransa waliokuwa wametekwa nchini Niger wawasili nyumbani

Rais Francois Hollande akiwa na mateka waliachiwa huru baada ya kuwasili jijini Paris

Raia wanne wa Ufaransa waliokuwa wametekwa nyara na kundi la Al Qeada lenye makao yake Kaskazini mwa Afrika nchini Niger wamewasili salama jijini Paris na kupokelewa na familia zao pamoja na rais Francois Hollande.

Raia hao walitekwa na kundi hilo mwaka 2010 nchini Niger na habari ya kuachiwa kwao ilitangazwa na rais Hollande ambaye aliahidi kuwapokea katika uwanja wa ndege.
Paris inasema kuwa haikulipa kikombozi kuwakomboa raia wake ambao wote ni wa kiume baada ya kusakwa kwa miaka mitatu bila mafanikio.
Kundi  hilo la al Qaeda linaloendeleza oparesheni zake Kaskazini mwa Afrika lilidai kuwa mwaka 2010 liliwateka Wafaransa hao wakati likipanga mashambulizi katika kampuni inayosimamiwa na serikali ya Ufaransa nchini Niger.
Rais Hollande amesema kuwa mateka hao waliachiwa bila ya nguvu zozote za kijeshi kutumiwa na kuongeza kuwa alipewa habari hizo na rais wa Niger Mahamadou Issoufou.
Aidha Hollande ameisifu serikali ya Niger kwa juhudi zake za kuhakikisha kuwa mateka hao wanaachiwa salama bila ya madhara kutoka mikononi mwa magaidi hao.
Ripoti zinasema kuwa raia hao wa Ufaransa waliachiwa baada ya msuluhishi Mkuu wa Niger ambaye wakati mmoja alikuwa mwaasi wa kundi la Tuareg Mohamed Akotey anayeheshimika sana nchini humo kuingilia kati.
Raia hao wa Ufaransa ambao wametajwa kama Thierry Dol, Daniel Larribe, Pierre Legrand na Marc Feret wameliambia shirika la habari la Ufaransa AFP kuwa wamefurahi mno kuwa huru lakini maisha yao chini ya mateka hayakuwa rahisi.
Wakati wa Oparesheni  ya kijeshi katika nchi jirani ya Mali, mateka hao wanasema walikuwa wanahofia maisha yao kwa sababu walifikiri wangeuliwa kama njiamojawapo ya kulipiza kisasi.
Hadi kutekwa kwao, raia hao wa Ufaransa walikuwa wameajiriwa na kampuni ya Uranium ya reva nchini Niger.

Tanzania: Tunaweza kujitoa A. Mashariki


Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Serikali ya Tanzania imesema inatafakari ushiriki wake ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na inaweza kujitoa ndani ya Jumuiya hiyo iwapo itaendelea kutengwa katika baadhi ya vikao.
Aidha imesema Tanzania haitambui vikao vinavyofanywa na nchi tatu zilizopo ndani ya Jumuiya hiyo ambazo zimekuwa zikizitenga Tanzania na Burundi.
Waziri anayehusika na masuala ya Afrika Mashariki wa Tanzania Samwel Sitta ameliambia Bunge la Tanzania kuwa makubaliano ya vikao hivyo vinavyofanywa na nchi za Kenya, Rwanda na Uganda yatatekelezwa na nchi hizo zinazofanya vikao hivyo kwa sababu vinafanyika nje ya utaratibu wa mkataba wa jumuiya hiyo.
Katika mikutano iliyofanyika hivi karibuni Tanzania na Burundi hazikualikwa kwenye vikao hivyo.
Kwa mujibu wa Waziri Sitta mikutano ya wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambayo ilianza kwa kuitenga Tanzania ilifanyika Entebbe nchini Uganda mwezi Juni mwaka huu na kufuatiwa na mkutano wa pili uliofanyika Agosti mwaka huu huko Mombasa nchini Kenya ambapo nchi hizo tatu bila kuishirikisha Tanzania walizungumzia uanzishaji wa himaya moja ya forodha.
Mambo mengine waliyozungumza wakuu hao ilikuwa uanzishaji wa visa moja ya utalii kwa nchi zao na matumizi ya vitambulisho vya uraia ambavyo vitatumika kama hati za kusafiria miongoni mwa nchi hizo.
Aidha Waziri Sitta amesema ndani ya mikutano hiyo pia walizungumzia kuanzisha mchakato wa kuanzisha shirikisho la nchi hizo.
Tayari Tanzania imeanza mazungumzo na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kuangalia ni kwa namna gani zitaanzisha ushirikiano nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama zinavyofanya nchi za Rwanda, Uganda na Kenya.

Marekani yaongeza juhudi kumsaka Kony

Joseph Kony, kiongozi wa kundi la waasi wa Uganda (L.R.A.)
Joseph Kony, kiongozi wa kundi la waasi wa Uganda (L.R.A.)

 


 
Ripoti mpya inasema Marekani imeongeza  juhudi zake  kusaidia kumkamata mtoro  kiongozi wa kundi la waasi wa wa Uganda Joseph Kony Kwa mujibu wa gazeti la  Washington Post jeshi la Marekani limeomba White House kuweka kwa muda mfupi ndege aina ya Osprey nchini Uganda.

Inasema ndege aina hiyo inaweza kutua kama helikopta na kupaa kama ndege kubwa na itasaidia wanajeshi wa Marekani kwa ushirikiano na wenzao wa Afrika kumsaka Kony katika eneo kubwa analodhaniwa kuwa amejificha na kubomoa kambi alizoweka .

Washington Post linasema endapo ombi hilo litakubaliwa, idadi ya wanajeshi wa Marekani nchini Uganda itaongezeka maradufu na kufikia 100.
Uganda inaongoza juhudi za ukanda huo kumkamata Kony ambaye kundi lake la waasi Lords’ Resistance Army, limehangaisha vijiji vya nchi za Afrika ya kati kwa miaka.

 Aidha gazeti hilo linasema majeshi ya Marekani yameongeza mafunzo kwa wanajeshi wa Sudan Kusini  na  Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, ambayo yanahusika na msako dhidi ya Kony anayedhaniwa kuwa amejificha huko Congo.

Jumatatu, 28 Oktoba 2013


Obama alijua nini hasa?

Bado mpaka sasa Rais Barack Obama na Shirika la Ujasusi (NSA) wanatafuta la kusema baada ya kudhihirika kwamba simu ya mkononi ya Kansela Angela Merkel wa Ujerumani ilikuwa ikitegwa na maafisa wa ujasusi wa Marekani.
Picha inayoashiria unasaji wa simu za Ujerumani uliofanywa na Marekani.
Picha inayoashiria unasaji wa simu za Ujerumani uliofanywa na Marekani.
Gazeti la kila Jumapili la "Bild am Sonntag" linalosomwa na watu wengi nchini Ujerumani jana (tarehe 27 Oktoba) liliripoti kwamba Rais Obama alijua kwamba simu ya mkokoni ya Kansela Merkel ilikuwa inasikilizwa na NSA tokea mwaka 2010. Shirika hilo limeyakanusha madai hayo, lakini bado pana hitilafu nyingi.
Ikulu ya Marekani imenyamaza kimya na NSA inasubiri. Msemaji wa Idara ya Ujasusi ya Marekani ameeleza kuwa ripoti ya "Bild am Sonntag" siyo sahihi. Mkuu wa NSA, Keith Alexander, hakumpa taarifa Rais Obama binafsi juu ya shughuli za kusikilizwa kwa simu ya Kansela wa Ujerumani na NSA. Pana madai kwamba Mkurugenzi wa NSA na Rais Obama asilani hawakuzungumzia juu ya shughuli za upelelezi zilizomhusu Kansela Markel.
Jambo moja linaweza kuwa wazi kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la New York Times , kwamba simu ya mkononi ya Kansela Merkel ilianza kusikilizwa na majasusi wa Marekani miaka 10 iliyopita au hata kabla ya hapo. Wakati huo Merkel bado alikuwa mwenyekiti tu wa chama cha CDU.
Aliyekuwa wakala mwaminifu wa NSA kwa muda wa miaka 18, Thomas Drake, ni mtu anayepaswa kuyajua ya jioni na ya asubuhi katika shirika hilo. Amesema hakushangazwa ni kilichotokea.
Kumbukumbu za Statsi
Picha hii ya tarehe 2 Septemba 2009 inamuonesha Rais Barack Obama akiwa na Kansela Angela Merkel kwenye mkutano wa kilele wa G20 jijini London.Picha hii ya tarehe 2 Septemba 2009 inamuonesha Rais Barack Obama akiwa na Kansela Angela Merkel kwenye mkutano wa kilele wa G20 jijini London.
Kutokana na kukasirishwa juu ya kupelelezwa kwa simu za wananchi wa Marekani , Drake angelikuwa mtoboa siri siku nyingi kabla ya Edward Snowden.
Ameeleza kuwa alikuwa anatarajia kuyasikia mambo mengine yakifichuliwa kutokana na kile anachokijua kutokea ndani ya shirika la NSA. Yaliyotokea pia yanamkumbusha enzi za zamani.
"Hebu kumbuka enzi za ufashisti nchini Ujerunmani. Hebu kumbuka enzi za upelelezi wa shirika la ujasusi la Stasi katika Ujerumani Mashariki. Yaliyofanyika kwa Angela Merkel yamemgusa sana yeye binafsi kukumbuka mashambulizi ya nchini Marekani, kwa sababu wateka nyara walikuwapo nchini Ujerumani, waliishi Ujerumani na walikwenda Marekani kutokea Ujerumani. Na kwa hivyo serikali ya Marekani na shirika la NSA kwa pamoja waliamua kuwa Ujerumani inapaswa kuwa kituo kikuu cha kupelelezwa barani Ulaya."
Wakala huyo wa zamani wa shirika la NSA ameeleza kuwa yanayoibuka sasa na kutokea hadharani hayasemeki.
Thomas Drake, ambaye alifanya upelelezi dhidi ya Ujerumani ya Mashariki ya zamani, amesema kilichotokea "kinamkumbusha enzi za Statsi na pia yanamkumbusha enzi za mafashisti nchini Ujerumani."
Mwandshi wa habari aliyefichua kashfa ya Watergate, Bob Woodward, pia amezikosoa shughuli za shirika la NSA.

Tullow yasitisha uchimbaji Turkana, Kenya

Kampuni ya Tullow inashirikiana na Afrika Oil kuchimba mafuta baada ya kuyagundua mwaka 2012
Shughuli ya uchimbaji mafuta katika jimbo la Turkana Kaskazini Mashariki mwa Kenya, imesitishwa baada ya totafuti kuibuka kati ya wenyeji wa eneo hilo na wakuu wa kampuni iliyopewa kandarasi ya kuchimba mafuta ya Tullow.
Tullow imesema imefunga visima vyake viwili vya mafuta kwa sababu ya hofu ya usalama kufuatia maandamano ya wenyeji wakitaka kupewa nafasi zaidi za kazi katika sehemu wanakochimba mafuta.
Wenyeji wa eneo hilo walifanya maandamano mnamo siku ya Jumapili kulalamikia hatua ya kampuni hiyo kutowapa ajira katika shughuli za uchimbaji na badala yake kuwaajiri watu wasio wenyeji wa eneo hilo.Kampuni hiyo kupitia kwa vyombo vya habari ilisema kuwa imesitisha Shughuli hizo kwa kipindi kisichojulikana hadi utulivu utakapororejea katika eneo hilo.
Shughili ya uchimbaji ilianza mwaka huu baada ya Tullow kugundua visima vya mafuta mwaka 2012 na inachofanya sasa ni kuangalia thamani ya mafuta ikiwa yanaweza kuleta mapato kwa nchi.
Aidha Tullow ilisema kuwa kumekuwa na maandamano ya mara kwa mara na kutatiza shughuli zake kuchimba mafuta. Baadhi ya viongozi katika eneo hilo wanaluamu wanasiasa kwa kuwachochea wakaazi kufanya maandamano na kuwa kwa sasa yamegeuka na kuwa ya vurugu pamoja na kutishia usalama.
Hata hivyo kampuni hiyo imesisitiza kuwa inashauriana na jamii za eneo hilo kuleta utulivu kwa njia ya amani kwani cha muhimu sasa ni kuhakikisha kuwa wafanyakazi wake hawadhuriki kwa vyovyote.
Wakaazi wa Kusini na Mashariki mwa Turkana walifanya maandamano kwa kile wanachosema ni kampuni hiyo kukosa kuwapa ajira na hata kandarasi katika shughuli nzima za uchimbaji.
Wakaazi hao walioongozwa na viongozi wao ikiwemo wabunge wakiituhumu kampuni hiyo kwa kuwahadaa na kuwanyima fursa za kazi huku wakikosa kutimiza ahadi yao ya kuhakikisha kuwa wakaazi hao wanapewa nafasi za kujiimarisha kiuchumi.
Hatua ya wakaazi ilikwamisha shughuli katika visima vya mafuta ambavyo viligunduliwa mwaka jana kuwa na uwezo wa kuzalisha viwango vikubwa vya mafuta. Wanataka kampuni hiyo kushughulikia kilio chao cha kuwapa nafasi za kazi.

G4S yatuhumiwa kwa ukatili Afrika Kusini

Kamuni ya ulinzi ya G4S imakanusha madai ya ukatili dhidi ya wafungwa
Wafanyakazi wa jela moja la Afrika Kusini la wahalifu sugu na ambalo linalindwa na kampuni ya ulinzi ya Uingereza G4S , wametuhumiwa kwa kufanya ukatili wa kiwango cha kushtua.
Serikali ya nchi hiyo sasa imeamua kudhibiti ulinzi wa jela hiyo ya Mangaung ya kuanzisha uchunguzi.
Hatua hii inajiri baada ya wafungwa kulalamiika kuwa kupigwa kwa nguvu za umeme na kulazimishwa kudungwa sindano hata hivyo G4S inakanusha madai hayo ikisema kuwa hakuna ushahidi kuwa wafanyikazi wake wanatekeleza vitendo hivyo.
BBC imepata video kutoka katika gereza hilo lenye ulinzi mkali ambapo milio ya nguvu za umeme inasikika .Inaonyesha pia mfungwa mmoja akikataa kupewa matibabu
Watafiti wa Wits Justice Project kutoka chuo kikuu cha Wits mjini Johannesburg wanasema kuwa wamekusanya ripoti za wafungwa karibu 30 kuhusiana na kupigwa kwa nguvu za umeme na kuchapwa katika utafiti wao wa mwaka mmoja
Mwandishi wa BBC Andrew Harding anasema kuwa serikali ya Afrika Kusini inasema kuwa hali katika gereza hilo lenye ulinzi mkali ya Mangaung ni ya kushtua sana
“Wengine walisema kuwa walizirai waliposhindwa kustahimili uchungu wa nguvu za umeme,” alisema Ruth Hopkins ,mwanahabari wa mradi wa Wits Justice
Alisema kuwa wafungwa walilalamika kuhusu kuvunjika kwa mikono na miguu na majeraha mengine makuu.
Mmoja wa aliyekuwa mfungwa kwa gereza hilo aliambia BBC kuwa nguvu za umeme zilitumika kuwatesa ,vilevile askari aliyefutwa kazi aliongezea kuwa wafungwa walimwagiliwa maji ili kuongeza uzito wa nguvu za umeme.
“Madai yoyote ya yakiripotiwa kwetu ,ambayo ni ya kesi ya kipekee inatubidi kuyashughulikia vilivyo”
Kulingana na mwandishi wa BBC wa Afrika Andrew Harding ,wakili wa baadhi ya wafungwa hao alishutumu tabia ya wafanyikazi katika gereza hilo kufanya ukatili bila kujali.
G4S hata hivyo imedai kuwa kuwepo na purukushani katika gereza hilo ni kwa sababu ya mzozo wa ajira. Zaidi ya askari 300 walifutwa kazi mwezi huu baada ya kushiriki mgomo
Nontsikelelo Jolingana,ambaye ni kamishna wa vitengo vya marekebisho aliambia BBC kuwa kitengo chake kimeanza uchunguzi rasmi kuhisiana na madai hayo .
Shirika la magereza ya Afrika Kusini mwezi jana lilitangaza kuwa wanachukua wanadhibiti ulinzi katika gereza hilo lililo katika mkoa wa Central Free State kwa muda baada ya shirika la kibinafsi la usalama kushindwa kulisimamia vyema gereza hilo.
Andy Baker, ambaye ni mkuu wa G4S Afrika alisema kuwa kuwadunga wafungwa sindano si jukumu la G4S bali ni la wafanyikazi wa afya.
Alipoulizwa kuhusu madai ya kutumia nguvu za umeme na kupigwa didhi ya wafungwa alisema kuwa “hakujawahi kutokea jambo hilo”

Jumamosi, 26 Oktoba 2013


Wanawake wa Saudi Arabia wadai haki ya kuendesha magari kama wanaume

Mwanamke wa Saudi Arabia akiingia katika gari
Mwanamke wa Saudi Arabia akiingia katika gari
www.cnn.com

Na Sabina Chrispine Nabigambo
Nchi ya Saud Arabia huenda ikakumbwa na maandamano leo Jumamosi baada ya wanaharakati wanawake kutangaza kufanya kampeni endelevu ya uendeshaji magari, kupinga marufuku ya wanawake kuendesha magari katika nchi hiyo ya kifalme.

Awali wanaharakati hao walitangaza kuzindua kampeni ya kuendesha magari leo Jumamosi lakini wameahirisha baada ya vitisho vya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yao,badala yake wametangaza kuifanya kampeni hiyo kuwa endelevu kuanzia leo.
Nchi ya Saudi Arabia ni nchi pekee duniani ambayo inapiga marufuku wanawake kuendesha magari na wanawake wanaokiuka marufuku hiyo hukamatwa na kufungwa.
Mwaka 2007 mfalme Abdullah alitangaz kuwa marufuku hiyo ni uamuzi wa kijamii uliofikiwa na raia wa nchi hiyo na hivyo serikali inatekeleza matakwa ya watu wake.
TAGS: SAUDI ARABIA

Nia njema haipo katika kushirikisha wazawa sekta ya gesi Tanzania-Mengi



Reginald Mengi

Reginald Mengi
UKUBWA WA HABARI 
Mkutano wa pili wa kimataifa wa masuala ya uendelezaji wa nishati ya  mafuta na gesi ulimalizika alhamisi jijini Dar es salaam Tanzania ambapo ulijumuisha serikali, taasisi za umma na makampuni mbali mbali.

Mwenyekiti wa taasisi ya sekta binafsi nchini Tanzania (TPSF)  Dkt. Reginald Mengi ambaye alikuwa ni mmoja wa watoa mada akizungumza na Sauti ya Amerika kuhusu pendekezo lake la kusitishwa ugawaji wa vitalu amesema hilo halikufanikiwa kwasababu kinachompa shida ni kwamba hakuna sera ya kugawa au kutoa vitalu.

Aliongeza kuwa wakati huo huo  vitalu hivyo vinatolewa kwa wawekezaji wa kigeni, alihoji  katika mkutano huo kuwa inakuwaje wagawe rasilimali za taifa bila sera maana ukifanya hivyo ni  uporaji tu. 
Alisisitiza  kwamba mtanzania hafaidiki  na hajaona chochote  cha kusema kwamba mtanzania atawezeshwa  kwasababu sheria ya mwaka 2004 inasema wazi wazi kwamba watanzania watawezeshwa kumiliki uchumi wao.

Kuhusu  mazungumzo yake na katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini Bw. Eliakimu Maswi  amesema hakukuwa na makubaliano ya aina yeyote ni mazungumzo tu , na tunapoendelea kuzungumza vitalu vinauzwa , kwahiyo haoni kama kuna nia njema kushirikisha wazawa wa Tanzania katika sekta ya gesi hasa katika ugawaji wa  vitalu.

Kutokana na kauli iliyotolewa na waziri wa nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo amemshauri arudi darasani akafundishe kwasababu anavyofikiria watanzania siyo wanafunzi wake darasani akiongeza kuwa mawazo yake hayana tija kwa wizara anayoongoza na wafanyabiashara wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Dkt.Mengi waziri huyo alikaririwa na vyombo vya habari nchini humo akisema kuwa wafanyabiashara wa kitanzania wanajua  biashara ya kuuza juisi tu jambo ambalo alisema ni tusi.

 Mkutano huo ulifanyika kutokana na  hatua ya hivi karibuni ya kugundulika kwa mafuta na gesi  nchini Tanzania. Waziri Muhongo akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni alisema hakuna Mtanzania mmoja mmoja atakayemiliki kitalu ila watanzania watawakilishwa na TPDC.

kadha wa Iran wauwawa mpakani



Msafara wa magari Saravan, Iran
Shirika la habari la taifa la Iran, IRNA, limearifu kuwa walinzi 17 wa mpaka wameuwawa katika mapambano na watu waliokuwa na silaha, kwenye mpaka wa Iran na Pakistan.
IRNA imeeleza kuwa baada ya shambulio hilo watu 16 wamenyongwa - watu wenye uhusiano na makundi yenye uhasama na serikali.
Kisa hicho cha mpakani kimetokea kwenye eneo la milima nje ya mji wa Saravan.
Washambuliaji hawajulikani, lakini mjumbe mmoja wa bunge la Saravan, Hedayatollah Mirmoradzehi, aliwaeleza hao kuwa magaidi wanaopinga mapinduzi.
Mpaka wa Iran na Pakistan huwa na machafuko na eneo hilo ni njia inayotumiwa na wafanya magendo ya mihadarati.

40 wauwawa Syria



Bomu lililotegwa katika gari nje ya msikiti karibu na mji wa Damascus limewaua watu 40 Ijumaa(25.10.20213),wakati afisa wa Umoja wa Mataifa ameeleza wasi wasi mkubwa kuhusu mamia ya watu ambao wamezingirwa.
A handout picture made available by Syrian news agency (SANA) shows a Syrian soldier carrying a wounded child to receivE first aid at Al Muwasat Hospital in Damascus, after injured at the site of a car bomb attack near Osama bin Zaid Mosque in Souk Wadi Barada in Rural Damascus, Syria, 25 October 2013. An official source told SANA that the explosion of the car led to the deaths of terrorists inside their car, and three citizens killed including a child, and 30 wounded, most of them in critical condition. As victims were being taken to the hospital, one of the injured people said, 'the explosion occurred before the end of Friday prayers and led to the collapse of the entrances of the mosque, damaging several shops and vehicles at the scene'. dpa/EPA/SANA HANDOUT /eingest. sc
Shambulio mjini Damascus , wamo watoto waliofariki
Mamia ya watu wamejeruhiwa katika shambulio la bomu lililotegwa katika gari katika mji wa Suq Wadi Barada, shirika lenye makao yake makuu nchini Uingereza la kuangalia haki za binadamu nchini Syria limesema, na ambalo linategemea mtandao wa wanaharakati na watu wengine ambao wameshuhudia matukio.
Serikali ya Syria na upinzani wamelaumiana kutokana na mauaji hayo. Suq Wadi Barada ni mji ambao unadhibitiwa na waasi na umezingirwa na majeshi tiifu ya utawala wa rais Bashar al-Assad.
Turkish soldiers take position in the southern border town of Akcakale on October 4, 2012. Turkish artillery hit targets near Syria's Tel Abyad border town for a second day on Thursday, killing several Syrian soldiers according to activists and security sources, after a mortar bomb fired from the area killed five Turkish civilians. Turkey's government said 'aggressive action' against its territory by Syria's military had become a serious threat to its national security and sought parliamentary approval for the deployment of Turkish troops beyond its borders. AFP PHOTO/BULENT KILIC (Photo credit should read BULENT KILIC/AFP/GettyImages) Wanajeshi wa kulinda amani
"Idadi ya watu waliouwawa kutokana na shambulio la bomu lililotegwa katika gari ambalo liliripuka baada ya sala ya Ijumaa katika mji wa Suq Wadi Barada imepanda hadi watu 40, ikiwa ni pamoja na watoto na wanawake," limesema shirika hilo la uchunguzi wa haki za binadamu.
"Idadi ya waliofariki huenda ikapanda kwasababu kuna watu kadha ambao wamejeruhiwa, wengi wao wako katika hali mbaya sana,"Limeongeza.
Magaidi wanahusika
Shirika la habari la Syria SANA , hapo kabla liliripoti kuhusu mripuko huo, na kulaumu kile lilichokiita kuwa ni "magaidi", neno linalotumiwa na utawala wa Assad kuwaelezea wapiganaji wanaojaribu kuuondoa utawala wake. Shirika la habari la SANA limesema "gari hiyo iliripuka wakati magaidi wakiwa wanaweka miripuko ndani ya gari hiyo ".
Kundi la muungano wa kitaifa wa upinzani wakati huo huo limeilaumu serikali ya Assad kwa mauaji yaliyosababishwa na kile ilichosema kuwa ni miripuko miwili ya mabomu yaliyotegwa katika magari yaliyowekwa nje ya msikiti wa Osama bin Zeid mjini Suq Wadi Barada. Mashambulio ya mabomu yaliyotegwa katika magari yamekuwa yakitokea mara kwa mara nchini Syria katika miezi ya hivi karibuni, na kuuwa watu kadha nchini humo.
Syrian in Zaatari, Flüchtlingslager in Jordanien
Place and date: 2012 Mafraq - Jordan
Copyright: Mohamad AL Anasweh - DW
via Hasan Hussain, DW ArabischWakimbizi wa Syria nchini Jordan
Televisheni ya Syria wakati huo huo imeripoti kuwa Abu Mohammed al-Jawlani , kiongozi wa kundi la al-Nusra Front , kundi la waasi lenye nguvu la Waislamu wanaofuata nadharia za jihad ambalo linamahusiano na al-Qaeda, ameuwawa kaskazini magharibi ya jimbo la Latakia, lakini kundi hilo baadaye limesema yuko katika hali nzuri.
Ghasia zaongezeka
Katika tukio jingine la ghasia shambulio la kushtukiza mashariki ya Damascus limewauwa waasi 24, limesema shirika hilo la kuangalia haki za binadamu nchini Syria , wakati shirika la habari la SANA limesema idadi ya waasi waliouwawa ni 40.
Maafisa wa Umoja wa Mataifa na wa Marekani wameeleza wasi wasi wao kuhusiana na eneo la Ghouta ya mashariki pamoja na maeneo mengine ya vitongoji vya mji mkuu Damascus ambavyo vimezingirwa, kufuatia ripoti kuwa kuna uhaba mkubwa wa chakula na kiwango ambacho kinaongezeka cha utapia mlo.
British Valerie Amos, United Nations Under-Secretary-General for Humanitarian Affairs and Emergency Relief Coordinator, launchs the Humanitarian Appeal 2011, during a press conference at the European headquarters of the United Nations in Geneva, Switzerland, 30 November 2010. EPA/SALVATORE DI NOLFI +++(c) dpa - Bildfunk+++Mkuu wa idara ya misaada ya dharura ya Umoja wa mataifa Valerie Amos
Mkuu wa idara ya Umoja wa Mataifa inayotoa misaada ya kiutu Valerie Amos siku ya Ijumaa (25.10.2013) amelitaka baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuweka mbinyo dhidi ya serikali ya Syria kuruhusu misaada kuingia katika eneo hilo ambalo lina wakaazi raia milioni 2.5 ambao wamekwama kutokana na mzozo huo.
Amos ameliambia baraza hilo lenye wanachama 15 kuwa "maneno , bila ya kuwa na uwezo wa kutoa msukumo, hayawezi kutengeneza picha ya madhila na mateso yanayotokea nchini Syria.

Ijumaa, 25 Oktoba 2013

Wapiganaji 40 wa upinzani wauwawa Syria

Wanajeshi wa serikali ya Syria leo wamewavamia waasi karibu na mji mkuu, Damascus, na kuwaua wapiganaji wapatao 40 wa upinzani. Mji wa kaskazini wa Safira, kusini mashariki mwa Aleppo, pia umeshambuliwa.
This image made from amateur video released by Ugarit News, which has been authenticated based on its contents and other AP reporting, shows smoke rises in Damascus, Syria, Friday, June 21, 2013. The commander of Syria's rebels confirms they have received new weapons, giving his forces more power in battles against government troops and Hezbollah fighters from Lebanon. Gen. Salim Idris refused to say in an interview with Al-Jazeera TV Friday where the weapons came from. (AP Photo/Ugarit News via AP video) Mapambano karibu na mji mkuu, Damascus
Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari uvamizi huo ulikuwa sehemu ya operesheni ya jeshi dhidi ya ngome za waasi zinazouzunguka mji huo, makao makuu ya utawala wa rais wa nchi hiyo, Bashar al Assad. Uvamizi huo karibu na Damascus umefanywa saa chache baada ya vikosi vya rais Assad kuuteka mji wa Hatitat al-Turkomen, kusini mwa mji huo, na hivyo kudhibiti barabara muhimu inayouunganisha mji huo mkuu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Damascus.
Shirika la habari la serikali, SANA, limesema waasi 40 wameuwawa katika hujuma hiyo iliyotokea karibu na eneo la Otaiba, na kwamba shehena kubwa ya silaha imepatikana, yakiwemo makombora ya kuripua vifaru. Eneo hilo ni sehemu ya ukanda unaojulikana kama Ghouta Masharki, ambako kulifanyika shambulizi la silaha za sumu mwezi Agosti mwaka huu, ambapo mamia ya watu waliuwawa, wakiwemo wanawake na watoto.
ATTENTION EDITORS - VISUALS COVERAGE OF SCENES OF DEATH AND INJURY Syrian activists inspect the bodies of people they say were killed by nerve gas in the Ghouta region, in the Duma neighbourhood of Damascus August 21, 2013. Syrian activists said at least 213 people, including women and children, were killed on Wednesday in a nerve gas attack by President Bashar al-Assad's forces on rebel-held districts of the Ghouta region east of Damascus. REUTERS/Bassam Khabieh (SYRIA - Tags: CONFLICT POLITICS CIVIL UNREST) TEMPLATE OUT Maiti za watu waliouwawa Ghouta na silaha za sumu
Afisa mmoja wa jeshi ambaye jina lake halikutajwa, ameiambia televisheni ya taifa ya Al-Ikhbariya kwamba wapiganaji wa kigeni ni miongoni mwa waliouwawa na shambulizi hilo limefanywa baada ya kupata taarifa za kijasusi. "Ilikuwa operesheni iliyofanikiwa. Tutaendelea kupata ushindi kutoka sehemu moja hadi nyengine," akaongeza kusema afisa huyo.
Mwanajeshi mwingine, ambaye hakutambulishwa kwa majina, amesema waasi ni wa kundi la Islam Brigade na Jabhat al Nusra au Al Nusra Front, lenye mafungamano na mtandao wa kigaidi wa al Qaeda. Shirika la haki za binaadamu la Syria lenye makao yake jijini London, Uingereza limesema wapiganaji wapatao 20 wameuwawa katika uvamizi huo, lakini halikutoa maelezo zaidi.
Wakati huo huo, helikopta za jeshi zimeushambulia mji wa kaskazini wa Safira, kusini mashariki mwa Aleppo. Kambi kubwa ya jeshi karibu na mji huo inaaminiwa ina kituo cha chini ya ardhi cha kinachotumiwa kutengeneza na kuhifadhi silaha za sumu. Shirika la madaktari wasio na mipaka limesema watu 130,000 wameukimbia mji wa Safria mwezi huu na kwamba mji huo umekuwa ukishambuliwa kwa mabomu tangu Oktoba 8. Taarifa ya shirika hilo imesema watu 76 wamekufa mjini humo.
Shambulizi la bomu
Katika tukio lengine la machafuko, shirika hilo limeripoti kuwa bomu lililokuwa limetegwa ndani ya motokaa limelipuka nje ya msikiti katika kijiji cha Suq Wadi Barada, na watu 40 ama wameuwawa au kujeruhiwa katika mlipuko huo. Hakuna taarifa za idadi kamili ya watu waliouwawa au kujeruhiwa katika mji huo, unaopatikana kaskazini magharibi mwa mji mkuu, Damascus.
Mkurugenzi wa shirika la haki za binaadamu la Syria, Rami Abdel Rahman, amesema miongoni mwa waliojeruhiwa ni watoto. Rahman aidha amesema ingawa mji huo uko mikononi mwa waasi, wanajeshi wanaomtii rais Assad wameuzingira. Televisheni ya taifa imeripoti juu ya shambulizi hilo, ikiwashutumu magaidi wenye mafungamano na al Qaeda. "Waasi wa kundi la Al Nusra Front wamelipua bomu karibu na msikiti wa Osama Bin Zeid katika kijiji cha Suq Wadi Barada katika mkoa wa Damascus. Taarifa za awali zinasema watu wameuwawa na wengine kujeruhiwa," ikatangaza televisheni hiyo.
Mapambano ya Wakurdi
Kuhusu mapambano kati ya Wakurdi na wapiganaji wa jihad shirika hilo limesema wapiganaji wa kikurdi wamezidi kusonga mbele katika mkoa wa Hassaekh wenye idadi kubwa ya Wakurdi. Wapiganaji hao waliingia mji wa Yaaroubiyeh leo na kukabiliana na makundi kadhaa ya jihad, yakiwemo Islamic State of Iraq na Al Nusra Front, yenye mafungamano na kundi la al Qaeda.
A Kurdish female fighter from the Popular Protection Units (YPG) carries a walkie-talkie as she stands near fellow fighters carrying their weapons and using binoculars in the Kurdish town of Ifrin, in Aleppo's countryside October 14, 2013. Kurds comprise around 10 percent of Syria's 23 million population. They are concentrated in Ifrin and other areas of the northwest, in parts of Damascus and in the northeastern oil producing area of Qamishli, where there has also been intense fighting between Kurds and al-Qaeda linked Islamic State of Iraq and the Levant fighters. Picture taken October 14, 2013. REUTERS/Roshak Ahmad (SYRIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST CONFLICT) Wapiganaji wa Kikurdi nchini Syria
Mji wa Yaaroubiyeh unaodhibitiwa na waasi uko katika kivuko kikuu cha mapakani kuingia nchini Iraq na kuuteka mji huo kutawapa wapiganaji wa Kikurdi njia rahisi ya kusafirishia bidhaa na mahitaji mengine kutoka eneo la Wakurid kaskazini mwa Iraq. Eneo hilo limeshuhudia mapiganao makali katika siku za nyuma na mapambano makali kati ya wapigaji wa Kikurdi na wapiganaji wa makundi ya jihad kaskazini mwa Syria yamesababisha vifo vya mamia ya watu katika miezi iliyopita.
Pia mwezi Machi mwaka huu wanaume waliokuwa wamejihami na bunduki waliwaua wanajeshi 51 wa Syria baada ya kuvuka na kuingia Iray kutoka Yaaroubiyeh. Wanajeshi hao walikuwa wameingia Iraq kutafuta hifadhi kufuatia mapambano na waasi upande wa Syria wa mpaka.

Pamoja katika ghadhabu

Baada ya madai ya kudukukuliwa kwa simu ya mkononi ya Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na idara ya usalama wa Taifa ya Marekani NSA, washiriki wa mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya wanataka hatua zichukuliwe.
Kansela Angela Merkel na rais Francois Hollande. Kansela Angela Merkel na rais Francois Hollande.

Ingawa suala la ulinzi wa data na uendelezaji wa uchumi wa digitali lilikuwa miongoni mwa ajenda za mkutano mkuu wa viongozi wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels Ubelgji, hakuna aliejua kuwa lingepata umuhimu wa kipekee kabla ya mkutano huo.
Lakini sakata la udukuzi wa mawasiliano ya simu ya mkononi ya Kansela Angela Merkel limebadili mambo, na washiriki wa mkutano wanataka hatua zichukuliwe. Hadi jioni ya Jumatano, Ufaransa na Ujerumani zilikuwa na mitizamo tofauti juu ya taarifa kuwa idara ya Usalama wa taifa ya Marekani NSA ilikuwa imeyadukuwa mawasialiano ya raia wa Ulaya.
Barroso ailinganisha NSA na Stasi
Baada ya udukuzi huo kumgusa Kansela Merkel mwenyewe, kila kitu kilibadilika ghafla, na sasa Berlin na Paris zimeungana pamoja katika kuelezea kughadhabishwa na udukuzi huo. Rais wa halmashauri ya Ulaya Jose Manuel Barosso, alikwenda mbali na kuyiita tabia ya Marekani kuwa ni ya kiimla.
Rais wa Halmashauri ya Ulaya Jose Manuel Barroso. \
Rais wa Halmashauri ya Ulaya Jose Manuel Barroso.
 
"Tunafahamu hapa Ulaya nini maana ya utawala wa kiimla, na tunajua kinaochotokea pale serikali inapotumia madaraka yake kuingilia maisha ya watu. Kwa hivyo hili ni suala muhimu sana siyo kwa Ujerumani tu bali kwa Ulaya nzima - haki ya faragha, na ulinzi wa taarifa," alisema Barroso akiilinganisha NSA na shirika la ujasusi la iliyokuwa Ujerumani Magharibi.
Pia katika bunge la Ulaya, Kansela Merkel amepata uungwaji mkono na pia shinikizo, kutafakari juu ya athari za udukuzi wa mawasiliano si kwake tu bali pia kwa raia wote. Mbunge wa chama cha Kiliberali FDP Nadia Hirsh amemtaka Kansela Merkel kuonyesha sasa kuwa anawajali raia wake na siyo hadi yeye ageuke mwathirika ndiyo aonyeshe kujali.
Schulz: Mazungumzo ya biashara huru yasitishwe
Martin Schulz, ambaye ni rais wa Bunge la Ulaya na anaepewa nafasi ya kumrithi Barroso kama rais wa Halmashauri ya Ulaya, yeye ametaka hata mazungumzo juu ya makubaliano ya biashara huru kati ya Marekani na mataifa ya Ulaya yasitishwe kwanza.
"Mimi naamini sasa laazima kuwepo na wakati wa kusimama na kutafakari. Ninapokwenda kwenye mazungumzo na naanza kuhofia kuwa wenzangu katika upande wa pili, tayari wanajua kupitia ujasusi, kile ninachotaka kusema katika majadiliano, hapo kunakuwa hakuna usawa tena.
Rais wa Bunge la Ulaya Martin Schulz .  
Rais wa Bunge la Ulaya Martin Schulz .
 
Kwa hivyo naamini laazima kwanza tuzungumze na marafiki zetu Wamarekani juu ya viwango tunavyopaswa kulinda," alisema mwanasiasa huyo wa chama Social Democratic SPD cha hapa Ujerumani.
Siku ya Jumatano, saa chache kabla ya taarifa za udukuzi julikana, bunge la Ulaya, lilikuwa limepiga kura kusitisha mkataba wa mfumo unaojulikana kama SWIFT, ambao kupitia kwake, taarifa za kibenki za raia wa Ulaya hukabidhiwa kwa Marekani.
Lengo la mfumo huu ni kupambana na ugaidi, lakini wabunge wengi waliona kuwa unakiuka haki za faragha. Kabla ya sakata ka udukuzi kura dhidi ya mfumo wa SWIFT haikuwa na madhara makubwa kwa sababu serikali nyingi ambazi zinafaa kuridhia hatua hiyo, zinathamini zaidi suala la usalma kuliko udukuzi, lakini sasa upepo umebadilika kwa kiasi kikubwa.
Mada nyingine zafunikwa
Kabla ya matukio ya hivi karibuni, wengi walitarajia mkutano wa kawaida. Wakati wa mkutano huo, viongozi walitarajia kupiga hatua katika majadiliano ya kuedeleza muungano wa kichumi na kifedha inagawa hawakutemegea kufanya maamuzi yoyote ya msingi.
Viongozi wa Umoja wa Ulaya wakiteta jambo wakati wa mkutano wa kilele wa Umoja huo.  
Viongozi wa Umoja wa Ulaya wakiteta jambo wakati wa mkutano wa kilele wa Umoja huo.
Hata hivyo, suala la wakimbizi, ambalo Italia ililiweka katika ajenda ni la muhimu zaidi kuliko udukuzi, kwa sababu ni jambo la kufa na kupona kwa wahamiaji. Licha ya hivyo, hakutarajiwi kuwepo na mabadiliko makubwa katika sera ya wakimbizi ya Umoja wa Ulaya, kwa kuwa mataifa ya kaskazini hayataki kujihusisha na wakimbizi kabisaa.
Lakini kwa kulinganisha na maafa katika bahari ya Mediterranean, wakosoaji wanauona udukuzi wa Marekani kuwa ni jambo hafifu, hata kama simu ya Kansela wa Ujerumani ilidukuliwa.

Maalim Seif: Nitaendelea kugombea urais Zanzibar


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, ametangaza azma yake ya kuendelea kugombea urais visiwani humo pamoja na ukatibu mkuu wa Chama chake cha Wananchi (CUF). Akizungumza wakati wa kutathmini miaka mitatu ya utendaji wa serikali ya umoja wa kitaifa visiwani Zanzibar hapo jana, Maalim Seif Sharif Hamad alisitiza kuwa, atastaafu siasa pale atakapoishiwa na nguvu mwilini, na kwamba licha ya watu fulani kumuona kuwa ni kizingiti kwa matakwa yao, hataacha nia yake hiyo ya kuwatumikia Wazanzibari. Kuhusu kugombea tena nafasi yake ya ukatibu mkuu katika uchaguzi wa CUF utakaofanyika mwakani na urais wa Zanzibar mwaka 2015, Seif alisema kuwa atatoka tu endapo wanachama wataamua kutomchagua tena. Maalim Seif alianza kugombea urais wa Zanzibar kwa mara ya kwanza mwaka 1995 baada mfumo wa vyama vya vingi kurejeshwa rasmi nchini Tanzania lakini ukitoa uchaguzi uliopita, mara zote amekuwa akilalamika kwamba anapokwa ushindi na akitangazwa mgombea wa chama tawala cha CCM kuwa mshind

...A Letter to My Wife...

Default Barua kwa Mke Wangu...

...A Letter to My Wife...


28th January 2019, Monday

Ni miaka miwili sasa imepita tangu tufunge ndoa na mke wangu, Asante. Binti mrembo na mcha Mungu. Mahali tulipokutana mimi na yeye ni hadithi ambayo nitaomba kuwasimulia siku nyingine. Ni katika zile sehemu ambazo mtu kamwe usingetegemea/tarajia kumpata binti mwenye haiba kama zake (We found love in a hopeless place…Rihanna Cc: BAK).

Kama nilivyokwisha eleza hapo mwanzo, zaidi ya urembo wake,ambao hauringii wala kuutumia vibaya kama wengine, ni binti mmoja mpole ajabu, anajua kujali na anajituma. Ni mchango mkubwa katika maisha yangu kwani hapa nilipofika kama sio mawazo na changamoto zake basi sidhani kama hata robo yake ningefika. Ama hakika wahenga hawakukosea waliposema, ‘kosea njia utaelekezwa, ila ukikosea mke…’

Naam, ni siku tena ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu na pia kumbukumbu ya miaka miwili ya ndoa. Ndoa tuliyofunga January 28, 2017 siku ya Jumamosi..still fresh in my mind. Ni siku ambayo kwa kawaida ya watu walio katika ndoa, tena ya ‘Kikristo’ walitakiwa kuwa pamoja wakimshukuru Mungu kwa mbali alipowafikisha.

Haikuwa hivyo kwangu. Wiki mbili kabla ya siku hii nilikuwa nimeshapanga na Zulekha (shombeshombe again!damn me) kukutana. Zulekha aliwahi kuwa rafiki yangu wa kike tulipokuwa chuoni. Ni binti aliyelelewa katika maadili ya dini sana. Very strict na kwa hiyo mahusiano yoyote ya kimapenzi na mwanaume asiye wa Kiislamu yalikuwa mwiko/kiwicho/taboo kwao.

Ila ukweli ni kuwa mapenzi hayafungwi na dini, hivyo tuliendelea kuwasiliana na tupatapo nafasi kufanya yasotupasa kufanya japo kwa siri kubwa. Baada ya kumaliza chuo, Zulekha alichumbiwa na kuolewa na Mkurya mmoja mfanya biashara aishiye Kimanzichana. Tuliendelea kuwasiliana na mara moja moja kucheza mechi za wizi pindi ambapo mumewe yupo safarini. Nami miaka minane mbele nilibahatika kumpata huyu mke wangu ambaye leo tunatimiza miaka miwili ndani ya ndoa.

Alinipigia simu kunijulisha kuwa mumewe amesafiri kwenda Geneva hivyo kama ningeweza niende walau tukumbushie kwani ulikuwa ni muda mrefu sana umepita tangu tukutane. Nami bila kumuwaza mke wangu nikamkubalia na kumjulisha kuwa ningesafiri Jumapili ya tarehe 27 kwa kisingizio cha safar ya kikazi Mtwara.

Na hivyo ndivyo nilivyomuaga mke wangu kipenzi. Alisikitika kuwa nisingekuwepo siku ya kuadhimisha miaka miwili ndani ya ndoa yetu changa. Ilinibidi kutumia one of those magic words, “Sorry babes, I will make it up to you when I come back.” Alinisaidia kupaki na kunisindikiza hadi Mbagala rangi tatu nikapande basi ili yeye arudi na gari letu nyumbani, an Audi A3 sportback, one of my favorites.

Nilipanda basi la Hamanju kuelekea Mtwara ingawa kondakta alikuwa akifahamu kituo changu cha ukweli. Hivyo tulikubaliana nikampa alfu kumi anishushe kimanzichana kituoni ambapo nilimkuta Zulekha akiningoja kwa hamu ndani ya ki-vitz alichonunuliwa na mumewe.

Tulienda hadi kwake ambapo hatukupoteza muda na kuanza kulicheza game kwani tulikuwa na zaidi ya miezi tisa hatujawahi onana kabisa. Ulikuwa ni mtanange wa kukata na shoka na mtoto kutotumwa dukani kwa takribani dakika hamsini hivi ndipo kipenga cha kwanza kilipopulizwa kuashiria muda wa mapumziko.

Uchovu wa safari, mgongano wa mawazo kwa jinsi nilivyomuacha mke wangu, pamoja na uchovu wa mechi vilichangia kuingia katika dimbwi la usingizi ambao kwa mara ya kwanza nahisi siku hiyo sikukoroma. Nilikuja kustuka nasikia maumivu makali kwenye paji la uso. Kufumbua macho nilikutana na sura ya Mkurya mwenye hasira kali akiwa kashikilia panga mkononi. Hasira yake tu ilinitosha kuzimia kwa hofu ila nilijikaza na kutaka kunyanyuka ambapo alinizaba na ubapa nikajikuta nimejikunyata pembeni mwa kitanda.

Kumbe Mkurya yule alipoaga anaenda Geneva alimaanisha tu anaenda zake Arusha ila kilichonikera mimi ni tabia yake ya ‘kutokutanguliza koti nyumbani.’ Wakati nakua babu alituhadithia kuwa zamani walipokuwa wakirudi kutoka safari za mbali iliwabidi wafikapo kijiji kimoja kabla ya nyumbani kutanguliza koti lake kwa mkewe kupitia mmojawapo wa watoto wa kijiji hicho kuashiria kuwa mwenye ynumba yu karibu. Hii ilimpa mke nafasi ya kusafisha nyumba na kama kuna kidumu ndani kuhakikisha kinaondoka na mke kujiandaa kumpokea mumewe. Walijua hali kama hizo hazina budi kutokea, ila haikuwa sababu ya kumfuamia mkewe.

Babu alituambia zama zetu zimebadilika lakini kutanguliza koti ni muhimu ila kwa kipindi chetu kutanguliza koti ni sawa na kupiga simu siku moja kabla ya kufika, “Mke wangu, kesho natarajia kuondoka hapa Arusha saa mbili asubuhi kurudi nyumbani.” Inatosha! Ghafla kabla sijaweza kuzama zaidi kwenye mawazo mwanaume yule alinvamia na kuanza kunikata vibaya mikononi na panga lile la kichwani ndilo lilinipoteza fahamu kabisa.


Back at home, Msongola…

Mke wangu naye alipokea simu iliyomtaarifu kuwa mumewe yu mahututi Muhimbili kutoka kwa namba asiyoifahamu na kabla hajamuuliza ni nani simu ilikatwa. Alipata shida kufahamu kuwa nilipata ajali au ni nini hasa kwani kwa kawaida huwa ni mvivu kuangalia taarifa ya habari mpaka nimlazimishe. Hivyo hakufahamu kama jana yake kulitokea ajali yoyote au la.

Aliondoka haraka na kuja hospitali ambapo alipoulizia kuhusu mgonjwa aliyeletwa usiku wa kuamkia tarehe 28 kwa ajali hakuna aliyempatia jibu. Kwa haraka alimpigia simu dr. Kindonga na kumuuliza kama amepata taarifa zozote kuhusu mumewe. Dr. Kindonga naye alimjibu hana taarifa na hawezi kufuatilia kwani alikuwa akijiandaa na mitihani yake ya mwisho ya Masters.

Baada ya kuhangaika sana alifanikiwa kufika mapokezi ICU na kuwakuta manesi ambao waliona aibu hata kumweleza baada ya kuwatajia jina langu. Walimwambia tu, “Yupo ndani!” bila kutaja sababu ya mimi kuwepo huko.
Alifika ndani na kunikuta nimefungwa bandeji uso mzima…


Kuanzia hapa anasimulia mke wangu kipenzi: mwallu

Moyo ulinipasuka na kushindwa kuelewa ni nini hasa kilimpata mume wangu Mentor. Sikuweza kumuangalia hata mara mbili kwani machozi yalinitoka ghafla. Nilijikuta nikianguka chini na kupoteza fahamu. Nilishtuka niko mikononi mwa nesi aliyejitambulisha kwangu kama Samira. Alinitaka nikaze moyo nikajue jinsi ya kumtibu mume wangu kwani kwa hali aliyonayo alinihitaji nikiwa hai kuliko mfu. Baadaye nilikuja kugundua Samira alikuwa very sympathetic kwa kuwa hakuwa amefahamu nini hasa kilimsibu mume wangu.

Nilijikaza na kwenda mpaka kitanda alicholazwa Mentor. Zaidi ya macho yake na pua zilizotiwa mirija kila sehemu, huko kwingine kulikuwa kumezibwa kabisa. Daktari alikuja na kujitambulisha;

Dokta: “Habari dada, naitwa Dokta Chrispin”

Mimi: “Shikamoo dokta, naitwa Asante. Dokta nini kimempata mume wangu?”

Dr. Chrispin
(Akakohoa kwanza): “Mh! Dada (ingawa kwa vigezo vyote angetosha kuwa babu yangu!), pole sana. Mumeo alipatwa na ajali. Alifumaniwa na kupigwa ndo unamuona ha… ”

Dokta Chrispin hakumalizia sentensi ile nikazimia tena kwa mara ya pili (ingawa ilikuwa ni afadhali kwani nilikuwa nipige ukunga wa kufa mtu). Nilishtuka nipo ofisini kwa Dr. Chrspin nimelala kwenye examination bed yake. Alikuja kunipima mapigo ya moyo na kunibembeleza huku kanikumbatia kifuani mwake. Nililia sana na baada ya kutulia ndipo aliponimalizia mkasa wote. Sikuamini kama mume wangu Mentor angeweza kufanya vile. Sikuamini kama katika siku zote basi ingekuwa siku ya kumbukumbu ya ndoa yetu. Sikuamini hadi nilipooneshwa jalada la Polisi likielezea kila kitu kwa kinaga ubaga.

Dr. Chrispin alinitaka niende nyumbani nikaongee na ndugu na jamaa ili kupanga mipango ya matibabu kwani gharama zake zilikuwa kubwa kiasi kutokana na majeraha aliyoyapata hasa kichwani. Nilichukua nguo zake nikaziweka kwenye begi ambalo nilikuwa nimemsaidia kupaki asubuhi ya jana yake na kurudi nyumbani.

Nilianza kuwapigia simu kaka zake. Kaka yao wa kwanza Laurian alishtuka kwanza ila baada ya kumuhadithia mkasa wote alinijibu kuwa hawezi kutoa pesa kwa ajili ya upumbavu wa mtu mmoja na isitoshe anajenga. Familia yake haiwezi kuishi nyumba ya kupanga. Alimalizia kwa kusema, “Huyo mumeo nilishamuonya mara nyingi sasa basi umalaya wake usiniletee umaskini kwenye familia yangu.”

Kaka Kabezi, ambaye baada yake ndiye Mentor alizaliwa, alikuwa mtu wa pili kumjulisha. Yeye kwa kejeli kabisa aliniambia, “Shem, afe tu tukurithi!”

Nililia sana usiku ule nikashindwa hata kula wala kunywa chochote. Ni bahati tu mtoto wetu Cedric alikuwa kwa bibi yake.

Nilijaribu kuwapigia wifi zangu walau wao wangeweza kunisaidia kwani walionekana zaidi kumpenda kaka yao na walikuwa karibu naye kuliko kaka zao wengine. Mawifi nao hawakuwa msaada wowote kwangu.

Wifi mkubwa, Suraya, aliniambia hatoweza kunisaidia kwani anajiandaa kwenda nje ya nchi asubuhi kesho. Wifi anayefuatia, Dora, sista du kweli alinijibu hatoweza kutoa chochote ila ataleta chakula hospitali na kuanzia siku hiyo akawa hapokei tena simu yangu. Wifi mdogo, tena afisa wa Jeshi la Magereza, aliniambia yuko radhi kwenda kumlipia mfungwa atoke gerezani kuliko kutibu Malaya. Na Malaya huyu ni kaka yao, mume wangu. Moyo uliniuma sana nikakosa cha kufanya.

Marafiki zake; Willian, Alfred, Livingstone, Salvatory, Shabani, Peter, Aneth, Arnold, Dotto, Mary, Christine na wengine wengi wote walijifanya kuwa bize au hawana uwezo wa kumsaidia ilhali hao hao walikuwa marafiki wake wakubwa akiwa mzima.

Wengine kama kina Alfred na Willian walidiriki kunitongoza kabisa kwa ahadi za kunisaidia. Nilimlilia Mungu na kumuomba aniepushe na jaribu hili. Nilimuomba anioneshe mlango mwingine wa kutokea kwani niliamini upo. Ukweli nilishindwa kuomba muda mrefu kwani niliishia kulia na kulala hapo hapo nilipo.

Huku hospitali Dr. Chrispin akaanza kunisumbua nifanye haraka kwani nikichelewa sana mume wangu hatapona hata akifanyiwa hiyo operation. Ikanibidi kwenda kumlilia Dr. Chrispin.


1st February 2019, Friday

Niliwahi hospitali kwenda kumhudumia mume wangu ambaye hadi wakati huo alikuwa amelazwa tu ICU bila matibabu yoyote ya ziada. Nilienda kumwangukia Dr. Chrispin kumuomba anisaidie. Nilikuwa nimekuja na ile Audi ya mume wangu nikamwambia dokta ikiwezekana achukue hiyo amtibu mume wangu na akipona tutamlipa fedha la asipopona basi aichukue gari hiyo. Dr. Chrispin alinijibu tu, “Dada, hizo gari zipo chache sana hapa nchini nitakuwa chambo cha kuibiwa na kuuwawa mimi.” Akakataa katukatu akaniambia; “Ila dada…ukinifikiria vyema nitakusaidia ” Hukuhitaji PhD kumuelewa mzee yule asiye na haya. Ila kwa muonekano pia wa sura yake alikuwa serious.

Nilirudi nyumbani kwa majonzi makubwa kwani dokta Chris ndo alikuwa tegemeo la mwisho katika matumaini yangu ya kumuokoa mume wangu kipenzi. Nilianza kutafuta ATM cards za mume wangu walau nikaangalie ana kiasi gani kimebaki benki na kama kinaweza kutosha kusaidia kulipia matibabu yake. Kumbe ndugu zake walipokuja kunisalimia waliondoka na kadi zote za benki. Ilikuwa ni kama wameshaamua ndugu yao afariki. Sikukuta chochote kwenye wallets zake ila wakati narudishia kadi nyingine kwenye wallet ndipo kikadondoka kikaratasi kilichokunjwa vizuri. Ilikuwa ni barua;

Mke wangu kipenzi,

Kama unaisoma barua hii ni dhahiri kuna jambo baya limenikuta. Na zaidi sana najua litakuwa linahusika na umalaya wangu. Najua kuomba msamaha sitakuwa nimekusaidia kwa lolote. Ila ni ombi langu unisamehe, zaidi sana kwa mzigo ambao nitakuwa nimekutwisha.

Umalaya wangu umeniponza mke wangu na kamwe nisingependa kosa langu hilo liwe mzigo kwako mke wangu. Jitahidi kuwataarifu ndugu zangu watakusaidia. Kaka zangu na dada zangu pamoja na marafiki zangu. Kwa bahati nzuri unafahamiana nao vyema mke wangu.

Pia unaweza kuuza hiyo audi yangu itasaidia kwa gharama zozote hata ikitokea nimefariki. Tafadhali mke wangu, nyumba hiyo niliiandikisha kwa ownership ya mwanetu ili kwa vyovyote vile ndugu wasijaribu kukuibia. Usiiuze.
Mke wangu kipenzi (hata sidhani kama bado nastahili kukuita hivyo!), kama yote yakishindikana tafadhali usifanye jambo lolote zaidi ya hilo litakalokufanya ujutie maisha mbeleni. Ni heri uniache nife kwa dhambi zangu kuliko kutenda dhambi nyingine kuniokoa mimi. Najua ulivyo mzuri mke wangu, Asante. Watakutongoza wengi wakati huu wakijua una shida, tafadhali sana mke wangu usiwakubalie. Narudia tena, ‘Ni heri nife kwa dhambi zangu walau nitakuwa mfano wa kutoigwa kwa wengine wenye tabia kama yangu.’

Jambo la mwisho mke wangu. Yote hayo yakishindikana rudi kwa Mungu wako unayemuamini na uniombee mke wangu. Hiyo ilikuwa moja ya sababu iliyonivuta kwako. Mlilie yeye akusaidie kwani hawa wa duniani wote wakishindwa kusaidia basi ama kwa hakika Mungu yule niliyekufahamu ukimuamini atakusaidia.

Nisamehe tena mke wangu na niombee msamaha kwa mwanetu Cedric ikitokea nimefariki.

Wako,
Mentor.”

Ilimaliza barua hiyo na kunifanya nijisikie mnyonge kuliko alivyotarajia mume wangu.

Ila jambo moja katika ile barua lilinitia moyo, alipoongelea imani yangu. Nikajiuliza I wapi imani yangu? Nikajilaumu kwa kwenda kutafuta msaada kwa binadamu. Nakumbuka nilipiga magoti pale pale na kumlilia Mungu kuwa mimi mja wake sikustahili adhabu na aibu kama ile. Ni kweli mume wangu nampenda kama ahadi yetu ya ndoa ilivyosema, ‘kwenye shida na raha’ . Nikamwambia Mungu kama kweli yu pamoja nami basi katika jaribu lile anipe mlango wa kutokea.

Kwa mara ya kwanza siku ile tangu ajali ya mume wangu niliweza kuomba muda mrefu bila kulia. Nilijihisi kama naongea naye uso kwa uso. Naam, Mungu hakupi jaribu lililo juu ya imani yako wapendwa kwani katika ndugu na marafiki zake wote nilioongea nao nilimsahau Felix. Huyu aliwahi kufanya kazi na mume wangu wizara moja wakati wameanza kazi baada ya kumaliza chuo. Yeye alisikia kwa watu kuwa rafiki yake amepata ajali akaja moja kwa moja nyumbani na kuniuliza kama nina shida yoyote nikamueleza kila kitu ila ukweli ni kuwa moyoni nilikuwa na wasiwasi asijekuwa kama wenzake akaanza kunitongoza pia.

Felix aliniambia yeye kama yeye asingeweza kunisaidia ila kuna Msambaa mmoja, Iggy, anamfahamu anaweka bond magari kama niko tayari tukaweke bond Audi ya mume wangu nipewe pesa ya kumtibu. Nilikubali na siku hiyohiyo jioni mume wangu alifanyiwa operation na Dr. Chrispin. Ilimchukua miezi minne kupona kabisa na kurudi nyumbani. Gharama ambazo kwa hakika hatukuweza kulipa hivyo ilibidi walichukue gari lake pamoja na cellica niliyokuwa nimenunua mwaka 2013 kwa mkaka mmoja hivi. Ingawa ni kama alinihonga kwa bei aliyoniuzia.

Ama hakika mke wa mtu sumu wapendwa ila pia Mungu ni mweza wa yote. Sikujua kama mume wangu katika hali ile aliyokuwa nayo angeweza kupona na kama ningeweza kupata msaada wowote.


Wasalaam wapendwa,

@Mentor & mwallu.

SOURCE: JAMII FORUM

NINI MAWAZO YAKO KATIKA BARUA HII TUANDIKIE HAPO CHINI

Alhamisi, 24 Oktoba 2013

Yaya Toure alalamikia ubaguzi viwanjani


ubaguzi umekuwa ukiwanyima raha wachezaji weusi
Kiungo wa kati wa Manchester City Yaya Toure ameonesha kughadhabishwa na kulitaka shirikisho la kandanda barani ulaya, UEFA kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya ushangiliaji wenye kuashiria ubaguzi wa rangi, baada ya kudai kuwa vilifanyika dhidi yake timu yao ilipotoka na ushindi wa 2-1 jijini Moscow
Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Ivory coast alisema alimlalamikia mwamuzi wa mchezo huo Ovidiu Hategan kuhusu kitendo hicho, alipokuwa nahodha wa timu yake.
Toure anafikiri kuwa pengine shirikisho la soka barani ulaya litachukua hatua ya kufungia uwanja kwa miezi au miaka kadhaa.
Mwezi May, UEFA ilitangaza kuchukua hatua kwa vitendo vinavyoashiria ubaguzi wa rangi kwa kufungia kwa muda mfupi viwanja iwapo ni kosa la kwanza, na kufunga moja kwa moja kwa kosa la pili sambamba na adhabu ya kulipa pauni 42,800.

Jumatano, 23 Oktoba 2013

Arsenal yashindwa kutamba nyumbani chelsea yapeta AC Milan yalazimishwa sare, Olympique de Marseille yaangukia pua

mchezaji wa Arsenal Ozil kazini
mchezaji wa Arsenal Ozil kazini

Klabu ya Arsenal imeshindwa kutamba nyumbani mbele ya wajerumani Borusia Dortmund kwa kukubali kipigo cha mabao 2 kwa 1 ikiwa ni mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, huku mshambuliaji wake Wilshare akipata jeraha na kutolewa nje ya uwanja.

Borusia Dortmund ndio ilikuwa ya kwanza kuliona Lango la Arsenal kupitia mchezaji wake Henrikh Mkhitaryan kabla ya Olivier Giroud kusawazisha na kuwa 1-1.
Dakika 10 kabla ya kipenga cha mwisho, Arsenal walionekana kuzidiwa kasi na mshambuliaji Lewandowski ambaye alipachika bao la ushindi.
Katika mchezo mwingine, Chelsea imeshinda ugenini mabao 3-0 dhidi ya Schalke 04 ya Ujerumani, Fernando Torres alipachika mawili na Eden Hazard moja.
AC Milan ya Italia imelazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Barcelona katika mechi ya Ligi ya Mabingwa usiku wa jana katika Uwanja wa San Siro.
Mchezaji Robinho alitangulia kuwafungia wenyeji bao dakika ya tisa, baada ya kupewa pasi kutoka kwa Kaka- lakini Lionel Messi akaisawazishia Barca dakika ya 24 kwa pasi kutoka kwa Iniesta.
Mechi nyingine, Steaua Bucuresti imetoka 1 - 1 na Basel, Olympique de Marseille ikafungwa 2-1 na Napoli ya Italia, FC Porto imelala 1-0 mbele ya Zenit Petesbourg, Austria Wien imefungwa 3-0 na Atletico Madrid huku Celtic ikashinda 2 - 1 dhidi ya Ajax Amsterdam.

Maisha ya watu millioni 800 hatarini

wanasayansi wameonya kuwa maisha ya zaidi ya watu milioni 800 kote duniani wanaoishi kando ya bahari yapo hatarini kutokana na bahari kuchafuliwa na moshi wa mafuta na gesi chafu.
Greenpeace Artic Sunrise
Shirika la Kimataifa la Green peace limekuwa mstari wa mbele kupambana dhidi ya uchafuzi wa bahari
Utafiti uliofanywa na wanasayansi umeonyesha kuwa kuchafuliwa kwa bahari ni athari za mabadiliko ya tabia nchi na ni kitisho kwa viumbe vya baharini.
Matokeo ya utafiti huo yaliyofanywa na wanasayansi 29 kutoka nchi 10 yametathimini pia kuwa mabadiliko ya tabia nchi yanaathiri maisha ya watu zaidi bilioni 2 wanaoishi kando ya bahari na ambao wanategemea kipato kinachotoka na shughuli wanazofanya baharini.
Kwa mujibu wa mtafiti na masuala ya elimu ya uhusiano wa viumbe na mazingira katika chuo kikuu cha Hawai huko Honolulu, Camilo Mora utafiti huo umebaini kuwa moshi unaotoka viwandani unachangia bahari kuwa na joto kali zaidi na kubadilika kuwa tindikali na hivyo kupunguza kiasi cha hewa safi katika maji ya bahari, mabadiliko ambayo yanakuja mara moja na haraka na kuharibu viumbe vya baharini.
Asilimia 70 ya eneo la bahari kutotumiwa
Mtafiti huyo ameliambia shirika la habari la IPS kuwa hadi kufikia mwaka 2100 asilimia 70 ya eneo la baharini halitafaa kwa matumizi.
Utafiti huo umetathimini hali ya sasa na ya baadaye ya moshi unaotoka viwandani utakavyoathiri viumbe vya habarini kama vile samaki, makaa ya mawe, wanyama wa baharini, mimea na viumbe vinginevyo.
Mvuvi akitoka kuvua samaki baharini. Mabadiliko ya tabianchi yameelezwa kuathiri upatikanaji wa chakula na hivyo kuyaweka hatarini maisha ya mamilioni.  
Mvuvi akitoka kuvua samaki baharini.Mabadiliko ya tabia nchi yameelezwa kuathiri upatikanaji wa samaki 
 
Kwa upande wake mtafiti kutoka taasisi ya kimataifa ya utaifiti iliyopo Stavanger nchini Norway, Andrew Sweetman amasema ni wakati sasa wa kuangalia na kukabiliana na hali hiyo kutokana na ukweli kuwa athari za mabadiliko ya tabia nchi yataanzia kwenye ukanda wa bahari kuelekea nchi kavu.
Uhaba wa chakula pia kuathiri wengi
Kati ya watu milioni 500 hadi 870 maskini duniani kote wapo hatari kukosa chakula na mapato kutoka habarini kutokana na athari hizo.
Wanasayansi hao wameeleza kuwa kuna athari nyingi zaidi zinazosababisha kupungua kwa viumbe baharini kama vile uvuvi holela, matumizi ya kemikali za sumu na uchafuzi wa bahari lakini utafiti huo ulilenga zaidi namna mabadiliko ya tabia nchi yatakavyoathiri viumbe vya baharini.
Hali ambayo amesema kuwa inaashiria namna watu wanavyovua samaki na viumbe vingine vya baharini kwa wingi zaidi ya kiwango kilichopo. China, Taiwan, Urusi, India na Japan zimetajwa kuongoza kwa uvuvi holela wa samaki duniani.
Uvuaji kupita kiasi wa samaki ni chanzo cha kupungua kwa samaki baharini.  
 Uvuaji kupita kiasi wa samaki ni chanzo cha kupungua kwa samaki baharini.
 
Alex Rogers mwanasayansi kutoka chuo kikuu cha Oxford Uingereza amesema dunina inashuhudia mabadiliko ya haraka yanayotokea na kuathiri viumbe vya baharini lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa inapaswa kutambua kwamba hali hii ikiongezeka italeta gharama kubwa hapo baadaye.
Mkurugenzi wa kituo cha kimataifa cha elimu ya sayansi baharini, Elizabeth Selig ametoa wito kufanyika juhudi za haraka kuokoa viumbe vya baharini kutokana na umuhimu wake kiuchumi lakini pia kiafy

Alex Ferguson amponda David Beckham

 
David Beckham na Sir Alex Ferguson
Aliyekuwa meneja wa klabu ya Manchester United ya Uingereza Sir Alex Ferguson amesema David Beckham alilazimika kuondoka katika klabu hiyo kutokana na tabia yake ya kujiona ni mkubwa kuliko meneja wake.
Katika kitabu kipya kuhusu historia ya maisha yake Ferguson amesema enzi za uongozi wake walitofautiana na Beckham kutokana na kumkosoa kuhusiana na kiwango chake katika matokeo ya ligi ya FA 2003.
Mchezaji huyo alionekana kuwa na msimamo unaoonyesha kujiona mkubwa na kutokubali maelekezo .
Furguson amesema kuwa tabia ya Beckham ilionekana kubadilika tangia alipomuoa mwanamuziki maarufu wa miondoko ya pop Victoria kutoka kundi la Spice Girls
"David ni mchezaji pekee ambaye nilimuwezesha kumuweka katika mazingira ya umaarufu wa soka kidunia, lakini sikufurahishwa na maisha ya umaarufu wake na hasa kujiona yeye ni bora zaidi' alisema Ferguson.
Ferguson amesema haijalishi ni Alex Furguson ama Pete the plumber, lakini mamlaka ni mamlaka tu, hangeweza kuwa na mchezaji ambaye haheshimu mamlaka,nadhan kama ni kuondoka ni bora alivyoondoka tu.
Beckham aliyeshinda mara sita katika ligi ya Premier ya uingereza,vikombe viwili vya FA na moja katika Champions League akiwa na klabu hiyo baadaye aliuzwa kwa Real Madrid kwa dola million 25 katika msimu wa joto 2003,kabla ya kwenda nchini Marekani kuchezea klabu ya LA Galaxy.
Sir Alex Ferguson yeye amestaafu mwezi May mwaka huu umeneja katika klabu hiyo ya Manchester huku akiwa ni miongoni mwa mameneja walifikia mafanikio makubwa katika historia ya kuiongoza timu hiyo.

PAMBANO LA SIMBA NA YANGA


 \
Baadhi ya mashabiki walizima kwa mshangao wa kilichokuwa kinaendelea uwanjani
Ama kweli kutangulia si kufika,au kama wanavyosema wakongomani kuwa KOKENDE LIBOSO,EZA KOKOMATE.
Usemi huo ulidhihirika hapo  kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada ya Mabingwa watetezi Ligi kuu soka Tanzania Bara Timu ya Yanga,pamoja na kutangulia kufunga bao 3 dhidi ya Simba hadi mapumziko,walijikuta wakiambulia sare ya bao 3-3 hadi Mwisho wa mchezo baada ya Simba kusawazisha bao zote katika Kipindi cha Pili.
Huku Simba wakiwa wamepoteana hasa idara ya Ulinzi,ilianza kuruhusu wavu wake kutikishwa katika dakika ya 14 baada ya Mchezaji wake wa msimu uliopita Mrisho Ngasa kutia chuma wavuni kufuatia pasi ya Didier Kavumbagu.
Lango la Simba lilikuwa matatani tena katika dakika ya 35 pale Mganda Khamis Kiiza alipoandika bao la pili kwa shuti la mguu wa kulia baada ya mpira uliorushwa na Mlinzi Mbuyu Twite kuparazwa kichwa na Didier Kavumbagu kabla ya kumkuta Mfungaji aliyeujaza wavuni.
Mganda huyo Khamis Kiiza almaaruf Diego aliandika bao la tatu kwa Yanga sekunde chache kabla ya Mapumziko kufuatia kazi nzuri ya Haruna Niyonzima alieyekokota mpira na kumpasia Didier Kavumbagu ambaye naye alimsogezea Mfungaji.
Huku Mpira ukienda Mapumziko Yanga wakiongoza kwa bao 3-0 ,baadhi ya mashabiki wa Simba walianza kuondoka uwanjani kwa kukata tama hasa kutokana na kiwango duni cha mchezo kilichoonyeshwa na timu yao,huku Mashabiki wa Yanga wakishangilia na kuwadhihaki Simba kwa kuonyesha kuwa wangeweza kulipiza kichapo cha bao 5-0 walichoshushiwa na Simba mwaka jana kwenye uwanja huo huo wa Taifa.
Kipindi cha Pili kilianza kwa Simba kuwapumzisha Abdul halim Humoud na Haroun Chanongo na kuwaingiza Said Ndemla na William Lucian,katika idara ya Kiungo,mabadiliko ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo hasa yaliyobadili sura ya mchezo baada ya idara ya kiungo ya Yanga kuanza kuzidiwa na kasi ya vijana hao ambapo katika dakika 53 Betram Mwombeki aliipatia Simba bao la kwanza baada ya pasi ya Mrundi Khamis Tambwe.
Dakika tatu baadae Mpira wa Kona uliopigwa na Ramadhan Singano ulimkuta Joseph Owino ambaye aliujaza wavuni na kuipatia Simba bao la Pili lililozidi kuwapa morali wachezaji na mashabiki waliokuwa wameamka upya.
Hatimaye Simba wakaweza kusawazisha katika dakika ya 83 kufuatia Beki Kaze Gilbert kujitwisha mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Mlinzi Nassor Masoud Chollo.
Kwa Matokeo hayo Simba sasa inashika nafasi ya tatu kwa kuwa Pointi 19 nyuma ya Azam na Mbeya City zenye pointi 20 kila moja lakini Simba imecheza mechi moja pungufu.
Nao Mabingwa watetezi Yanga wako nafasi ya nne kwa kuwa na pointi 16.
Hakika lilikuwa Pambano ambalo Yanga walijiamini kuwa wameshinda kwa kutangulia kuongoza bao 3-0 ambalo si kawaida katika mechi za watani hao wa jadi katika Soka la Tanzania,na ndiyo Maana Simba walishangiliwa kwa nguvu kana kwamba wameshinda baada ya Kutoka nyuma na kusawazisha bao tatu.
Kwa upande mwingine mashabiki wengi walianguka na kuzimia ama kwa kushangilia matokeo au mshtuko kutokana na kutoamini kilichokuwa kinaendelea uwanjani hapo.
Kwa upande mwingine kukamilika kwa mechi hiyo kunafanya maisha yaendelea kama kawaida baada ya tambo za kila upande kwa takriban zaidi ya wiki moja ambapo mashabiki wa pande zote walikuwa wakitambiana kuwa kila mmoja timu yake ingeshinda Pambano hilo ambalo kwa kawaida huwagawanya mashabiki wa nchi hii pande mbili.

Facebook yaondoa picha zinazoogofya

 
Facebook yazuia picha zenye kuogofya
Siku chache tu baada ya mtandao wa Facebook kusema kuwa utawaruhusu watu kuweka filamu za video zinazoonyesha ghasia,imeondoa filamu moja ya video ya mwanamke anayekatwa shingo.
Tangazo hilo la hapo jana kwamba itaondoa marufuku hiyo kwa mda,miongoni mwa video za ghasia ilizua malalamishi mengi kutoka kwa uma.
Facebook sasa imesema itapanua vigezo vyake ili kubaini iwapo filamu za video zitawekwa katika mtandao huo au la.
Mwandishi wa BLOG hii anayesimamia maswala ya Technologia amesema hatua hiyo inawakilisha mabadiliko muhimu yalioshinikizwa na uma

Jumapili, 20 Oktoba 2013

Picha 5 za yule shabiki Steven wa Yanga alielia, akijiandaa kwenda kwenye mechi leo



3Ni shabiki mkubwa wa Yanga ambae alipata zaidi ya shilingi milioni 4 kwenye miezi miwili ya kwanza baada tu ya kuonekana kwenye TV akilia kwa uchungu kisa Yanga imefungwa tano, zikiwa ni pesa kutoka kwa watu mbalimbali ambao walimuonea huruma na wengine kujisikia tu kumpoozesha.
Ni muda umepita toka hiyo mechi ambapo leo tena Yanga na Simba kwenye uwanja wa taifa zinakutana ambapo Steven alipita mbele ya Camera ya millardayo.com na kuzungumza machache kuhusu hii mechi ya leo.
‘game ya leo ni nzuri japo maandalizi tumeshaanza muda mwingi sana tumejiandaa vizuri kwa hiyo tunategemea na sisi kupata ushindi sana, hatutegemei kama tutaipoteza hii game’ – Steven
Leo mkifungwa utalia tena?  ‘leo nikifungwa ndio nitazimia moja kwa moja na kuna uwezekano nikaihama hata club kwa sababu imani yangu iko hapa tayari kwamba tutashinda ila tukifungwa tena nitaachia ngazi kistaarabu, nitamuandikia barua Muheshimiwa Manji manake yeye ndio alinipa cheti cha heshima cha uwanachama wa Yanga, kuhusu club gani nitahamia hiyo ni siri yangu’ -Steven
‘Yanga sasa hivi tuko kiprofeshino kama Barcelona sasa hivi au Real Madrid, Simba tutaiona manake imesajili sana mwaka huu kama kina Tambwe…. kwa hiyo tunategemea maushindi zaidi utakuepo, tena ushindi wa mawili kwa moja au moja bila… si hatuhitaji magoli matano, tunahitaji pointi tatu tu’ – Steven
21
4
5