Heshima mbele!!
Sijui niseme nimebahatika,au nina bahati mbaya,ya kushuhudia watu watano kwa nyakati tofauti wakikata roho.
Huu ndio uzoefu wangu:
1: Babu yangu alikata kauli kama siku nne hivi.
Siku ya tano akapata faham,tukaongea naye,na alikuwa mchangamfu mno,akituasa sana kuishi vema.
Baadaye akasema ana usingizi.
Akajifunika shuka.
DOKTA alipo kuja dk. Kumi baadaye akatuambia tutoke nje,
punde akatuambia babu ametutoka.
2: Ndugu yangu mwingne.
Alilazwa kwa siku tatu.
Akasisitiza sana mwanae aitwe.
Mwanae alipo fika tu,akamkumbatia,
alipo lala,kesho yake tukaambiwa kafariki.
3: nimewah lazwa hosp,na kuna ndugu alikata roho pembeni ya kitanda changu.
Alihangaika sana kwa kurusha miguu,kujitingsha etc kabla ya kukata roho.
Haya ni ambayo nimeshuhudia.
Lakini kuna tales nyng zingne walizo ona wengine.
SWALI:
Nini hasa hutokea kwenye mind ya mtu kabla ya kukata roho&anapo karibia kukata roho?
Karibuni.
By Pasco:
Hii ni situation inaitwa "near death experience!" ambayo hutokea kabla ya kifo, wakati ambao roho inaacha mwili!.
Nitawahadithia kidogo experience yang na kuwapa za wengine!.
Niliwahi kupata ajali mbaya sana ya pikipiki, ikasemekana "nimekufa!", nikafunikwa kanga, na kuachwa wakisubiriwa polisi kufika kuuchukua mwili!. Kwa kawaida nikikumbuka huwa napata "stigmata" hivyo subirini nipate kidogo, ndipo nije nihadithie, ilikuwaje hatimaye nikawa hai tena1, na mpaka leo mimi nipo!.
.
By hippocratessocrates:
Sijui kama nitakujibu au nitakuwa nje ya mada/swali.
"Kukata roho"..ni neno/msemo tunaoutumia kila leo pale mtu anapokuwa anakuwa/ameacha kupumua na hapa ni zaidi ya kupumua, moyo kutofanya kazi, na viungo vingine vya mwili vikiwepo mapafu, ubongo n.k
Hii ni tofauti kidogo na ile watu wanapoita yuko katika 'Coma/Brain dead'.
Kwa kawaida mwili wa mwanadamu hutegemea msukumo wa damu, hii ikiwa kupitia damu hewa safi na chafu husambazwa mwilini na hata viungo vingi mf. misuli kutegemea nguvu(sukari) kupitia damu hii hii.
Kimabadiliko ya mwili, mtu anapokaribia kukata roho vitu hivi hutokea.
Kupungua kwa shinikizo/msukumo wa damu kwenda sehemu mbalimbali za mwili, hapa namaanisha upungufu wa lishe, hewa safi, na uongezekaji wa taka mwili ambazo zingepaswa kusafishwa.Hii hupelekea
1. 'Kuchanganyikiwa'
Ubongo unapokosa hewa safi, hufanya mtu kuona/kusikia(HASA KUONA) vitu tofauti na wengine. hapa utasikia watu wakisema "eee, marehemu alisema kabisa malaika amekuja kumuijia", au " alituaga kabisa kuwa anaenda mbinguni" n.k
2.Mwili kuwa wa baridi:
Msukumo mdogo wa damu husababishwa upungufu/uwezo mdogo wa mwili katika utoaji wa taka mwili, lakini zaidi hata urudishwaji wa damu ili isafishwe huwa mdogo zaidi.
3. Mwili kutoka jasho, kuhangaika:
Wakati kukiwa na uwiano mdogo wa hewa safi na msukumo wa damu, Bado mwili hujitahidi kutengeneza/kufanya njia za kutafuta uwiano huo kuwa sawa! Hapa mtu atahangaika kuwa kama 'hewa haitoshi', na wakati fulani kutokana na msukumo kidogo ambapo kupitia damu nguvu(sukari hupatikana), mwili hutengeneza sukari(nguvu) mbadala pia kupitia misuli, ambayo kupitia kwayo, jasho pia hutengenezwa/kuzalishwa.
5. Kujisaidia/Kupata haja:
Wakati mwili pia ukiendelea "kuhangaika" kupata nguvu/nishati, baadhi ya 'sphincters' kutegemea nguvu hii au kwa ajiki ya kujikakamua, hasa katika kibofu cha mkojo na mwishoni mwa mfumo wa chakula, hujikuta vikipitisha choo kikubwa/kidogo au vyote.
Haya ni baadhi tu ya MENGI yanayotokea wakati mtu anapokaribia "kukata roho"
By Pasco:
Nimerudi naomba nianze kama ifuatavyo
Kuzaliwa na kifo ni sehemu mbili muhimu sana kwenye maisha ya mwanadamu, kuzaliwa ikiwa ndio mwanzo wa maisha na kufa ndio mwisho wa maisha, kama ilivyo kanuni ya kila lenye mwanzo lina mwisho, hivyo hakuna chochote cha kustusha au kustaajabisha kuhusu kifo kwa sababu tangu ile siku ya kwanza binadamu anazaliwa, ni hakika anajua siku ya siku itafika na atakufa!.
Binadamu ana sehemu kuu mbili, mwili na roho ambayo ndio huo uhai. Kwa mfumo wa imani, mwili umeumbwa kwa udongo, hivyo tumetoka mavumbini, na ni mavumbini tutarudi!. Baada ya kuumbwa kwa udongo, Mungu akatupulizia pumzi ya uzima, huu ndio uhai, hii ndio roho, hivyo mtu anapokufa, kinachokufa ni mwili tuu, roho haifi, bali roho huuacha mwili!, (inakwenda wapi- tembelea Life after death: What Happens After Death? - Jamii Forums). Kitendo cha roho kuuacha mwili, ndicho hicho kiitwacho, kukata roho!, na huo ndio mwisho wa uhai wa mwili, hiyo roho ikiisha uacha mwili, huendelea na maisha mengine, mbinguni, motoni, peponi, ahera, jehanum, kwenye reicarnation, spiritual world, etc!.
Hili la Mwili na Roho, "physical body" na "spiritual body" nimelieleza kwa kirefu katika mada yangu hii Psychic Powers: Ni Nguvu za Kufanya Miujiza. Wengi wanazo bila Wao Kujijua...nimesema hivi
Kuna aina nyingi za roho kuacha mwili, usingizini, kwa uzee, kwa kuugua, kwa kuuliwa, kwa kujiua au kwa ajali. Hivyo pilika pilika za roho kuacha mwili mara nyingi zinategemeana unakufaje, umejiandaaje kufa, na umejaaliwa kiasi gani kufa kifo chema!.
Kwa wanaokufa kwa kuuliwa, au ajali, mara nyingi hutegemea injury iliyosababisha kifo huanzia wapi, ikianzia kwenye brain au kwenye moyo, then kifo ni instant, there and then!, bila maumivu yoyote na bila kukura kakara zozote, na ndio maana wadunguaji, hulenga kichwa au moyo, na utekelezaji wa hukumu za kifo za kisasa au mtu atapigwa risasi ya moyo, au atachomwa sindano ya sumu kuusimamisha ubongo!, no pain!. Kunyongwa ni unyama!.
Kwa vifo vya uzee, mara nyingi hutokea usingizini, na hawa wazee huwa wamejiandaa kufa, na kuna wengine kutoka na kuzeeka sana, wanamuomba Mungu, awachukue tuu wasiendelee kuwa mzigo kwa waliobaki, hivyo wengi huita watoto wao, huwapa usia, na kusubiria tuu siku ya siku na hawa hawana kutapatapa kwa sababu wame accept death!. Ukiona anaekufa kwa uzee anatapatapa, ujue huyo ama haja accept, au anateseka kufidia mambo fulani mabaya aliyoyafanya wakati wa uhai wake hivyo malipo ni duniani, kama hajafa hupata mateso kufidia, na mateso hayo ndioko kule kutapatapa huwezi jua endaikawa anakula bakora ila nyinyi hamzioni!. "Ila pia kuna wazee ambao wamekataa kukiruhusu kifo, bado wanaishi ila ni katika miili mingine na mahali pengine!"
Wanaokufa kwa ugonjwa nao ni kama wanaokufa kwa uzee, wale wanaoaccept kifo, hufa kimya kimya usingizini, wale wasiokubali matokeo hutaka kulazimisha kuishi, ila ugonjwa tuu wenyewe as ugonjwa ni mapigo, hivyo akitapatapa ujue anamalizia kufidia, hizo pia ni bakora!.
Kwa wanaokufa kwa kuuwawa, au kwa ajali, hawa wanakuwa hawajajiandaa kufa!, hivyo kifo kwao ni unexpected, mtu anaweza kuwa amekufa mwili, ila roho yake bado haijaenda mbali na mwili, hivyo anaona na kuyasikia yote yanayoendelea, sometimes hadi mwili unaposhushwa kaburini, ndipo roho huondoka!. Kwa vifo vingi vya ajali ambavyo miili haikupatikana kufanyiwa mazishi rasmi, baadhi ya roho hizo hubaki zikitangatanga na ndizo mizimu, ama huwatokea watu etc, zinaitwa Ghosts auWandering Spirits, unaweza kunisoma hapa kuhusu hawa "wondering spirits! hapa!, "Psychic Powers: Ni Nguvu za Kufanya Miujiza.
Kisa changu. Mimi ni" bike lover" siku zote usafiri wangu ni bike, ninazo pikipiki 6!, tano kati yake ni big bikes over 750cc!, Mbili nimenunua bongo, tatu niliziagiza, moja niliifuata!. My last bike ni big flying machine aina Harley Davidson "Buel" Firebolt 1200 CC niliinunua US, bongo ilikuwa the one and only na mpaka leo sijabahatika kuona hiyo kitu kwenye streets za bongo, hivyo huwa ninakwenda nayo popote, I simply fly!. Speed yake ni 240kph!.
Wakati maonyesho ya 88 yakifanyika Morogoro, mimi nilikuwa nalala Dar, asubuhi na paa zangu kwenye Moro ni 1:45 hour ride! na jioni narudi Dar!. Dar -Dodoma ni 3:45 hours ride. Dar-Moshi ni 4 hour ride, Dar-Arusha 5hrs ride!, I was simply mad!. Mind well, my wife and my bog boys wote wana drive magari yao, to me bike was my choice for convenience!, hivyo I don't regret what happened to me na bike ilichonifanya!. Na nimefanya safari za hivyo mara kibao!.
Nimeisha onya mara kibao, hatari za kusafiri na bike long distance, sikusikia!. Ukipenda mno bike, unakuwa kama kichaa fulani hivi, husikii mpaka yakukute!. Siku moja nikitoka Dar-Dodoma, nikiwa mwendo wa 160kmh, nilipata ajali mbaya, nikabingirishwa nilipoangukia, ikawa ndio hapo hapo!. Sikujitambua tena mwili, bali nilisikia tuu sauti za watu wakisema, huyu jamaa ameishakufaa hapa hapa!. Nakasikia watu wakisema leta kanga tumfunike, tungojee polisi waje kuuchukua mwili!. From then, sikujua tena nini kilichoendelea!.
Kumbe huku nyuma kuna dereva mmoja wa TAMISEMI naye ni bike love, alikuwa akiipenda sana bike yangu na mara kibao tunapishana Dar-Dodoma. Sasa alipoona ile bike, akaijua na kuuliza huyu jama yuko wapi, akaambiwa kafa pale pale!, akapelekwa kuonyeshwa mwili ulipofunikwa!. Kwanza aliipiga picha ile bike kwa simu yake, kisha akaupiga picha mwili wangu ukiwa umefunikwa. Kisha akasema huyu mwenye piki piki, namfahamu, naomba kumfunua kujiridhisha kama ndiye yeye!, akaifunua ile kanga, kuniangalia akakuta ndiye!, akawauliza umepita muda gani, maana hata damu ilishaanza kuganda, wakamwambia nusu saa!. Akanigeuza kunipiga search akakuta simu, akapiga home na kuwaeleza alichoelezwa!. Sasa katika huko kunigeuza ndipo akasema mbona mwili bado wa moto?!, akanisikilizia kwa karibu akasikia napumua kwa mbali!.
Akasimamia nikabebwa kuwahishwa Dodoma hospital, kwenye pochi wakakuta kadi yangu ya AAR, wakawapigia, mimi kuja kuzinduka ni saa 6 za usiku, nimezungukwa, wife ndugu, waandishi wa Dodoma, polisi, ndipo nikakumbuka kilichotokea na zile sauti za mfunikeni!.
Tangu niliposikia zile sauti za mfunikeni, kimoyo moyo nikajisemea I can't die!. No way!. Kumbukumbu zikapotea mpaka nilipozindukia hospital!. Ndipo nikaambiwa baada tuu ya ajali, walikimbilia kuniokoa, wakakuta sipumui wala sitingishiki, hivyo wakajua nimekufa!.Jamaa akanionyesha zile picha!.
Japo kifo ni kweli kimeumbwa, ukijiandaa na kukubali kufa, unakufa!. Ukisema no to death, no matter umeumia kiasi gani, you might live!. Dodoma wakashauri wafanye amputation ya baadhi ya viungo!, AAR wakazuia, kesho yake asubuhi nikaletewa charter na kuwa flown to Muhimbili, bima yangu ilikuwa ndogo, ingekuwa kubwa ningepelekwa Nairobi. Pale Muhimbili, wakajitahidi walivyoweza, nikapelekwa South huko bili ikawa too much to bear, nikahamishiwa India, japo sikupona kabisa, but I'm still alive!.
Naombeni msiniulize maswali yoyote kuhusiana na hii ajali, ninapata tatizo liitwalo "stigmata" hivyo kurudiwa na maumivu makali!, ila mimi ni miongoni mwa hao tuliopitia "near death experience!".
Asanteni.
Reply
By Apolinary:
Swali lako gumu kulijibu.
Labda waliowahi kukata roho kama wangekua wanarudi kutuambia nini kilitokea. lakini katika hali ya kawaida huwezi kujua ni nini kinatokea pindi Binadam anapouacha Uhai!
Mkuu Apolonary,ni gumu,ila naamini linajibika.
Tuna magwiji wa philosophy,medicine na religious experts humu.
Tusubiri tuone.
Reply
Labda ujaribu kwanza then unaweza kutupatia jibu zuri maada watafiti jufanya majaribio
\
Reply
Mmh maswali mengine bwana, sijui mlengwa ni nani hasa....kuna maswali marahisi ambayo majibu yake ni magumu kama ni nini kinatokea muda mfupi kabla ya kuzaliwa na magumu ambayo majibu yake ni magumu pia kama hili lako la sasa!
Reply
King'asti
Hili Ni suali la msingi Sana. Huwa najiuliza Sana kuhusu hili.
Reply
Money Stunna
Ilo swali gumu kuna mjomba wangu mwaka juzi alituita caracas venezuela hakatuaga na kutoa wosia .
Usiku huo hakafariki ninachoshangaa mbona wengine wanajua siku yao
Reply
Sista
jamani mbonamnatutisha? wengine tuna roho nyepesi
Reply
Bujibuji
Hebu tufanye umwiliisho (reinarnation) Reincarnation - Wikipedia, the free encyclopedia
Reply
kinyoba 18:35 19th February 2014
Naskia roho inapokutoka lazima kimba kidogo kikutoke.. Waswahili wanakuambia inaitwa NGAMA. Yaani cha mwisho kabisa! Ndio maana hata lugha za mtaani utasikia neno NGAMA.. Yaani cha mwisho kabisa alichobakiwa nacho!
Reply
Pasco
Hii ni situation inaitwa "near death experience!" ambayo hutokea kabla ya kifo, wakati ambao roho inaacha mwili!.
Nitawahadithia kidogo experience yang na kuwapa za wengine!.
Niliwahi kupata ajali mbaya sana ya pikipiki, ikasemekana "nimekufa!", nikafunikwa kanga, na kuachwa wakisubiriwa polisi kufika kuuchukua mwili!. Kwa kawaida nikikumbuka huwa napata "stigmata" hivyo subirini nipate kidogo, ndipo nije nihadithie, ilikuwaje hatimaye nikawa hai tena1, na mpaka leo mimi nipo!.
Pasco.
Reply
Myakubanga
By Pasco:
Hii ni situation inaitwa "near death experience!" ambayo hutokea kabla ya kifo, wakati ambao roho inaacha mwili!.
Nitawahadithia kidogo experience yang na kuwapa za wengine!.
Niliwahi kupata ajali mbaya sana ya pikipiki, ikasemekana "nimekufa!", nikafunikwa kanga, na kuachwa wakisubiriwa polisi kufika kuuchukua mwili!. Kwa kawaida nikikumbuka huwa napata "stigmata" hivyo subirini nipate kidogo, ndipo nije nihadithie, ilikuwaje hatimaye nikawa hai tena1, na mpaka leo mimi nipo!.
Pasco.
Rudi mkuu Pasco
Reply
Mtokambali
Nafikiri hata kwa wale tuliowahi kufanyiwa operesheni ukiwekewa ile dawa wanaita nusu kaputi unahama ulimwengu huu,ule si usingizi bali nusu ya kifo. Kwa kawaida mambo unayoongea wakati ukipotelea usingizini na yale utakayoongea au kufanya ukiwa unarudiwa fahamu huwa ni sawa na experience ya mtu anayekufa aise. Na muda wote wa huo usingizi mzito huwa ni kama kifo japo unapumua,ubongo wako unakuwa umeonja mauti....
Reply
Sista
mada nzito hiiii
Reply
bunited
we c ajabu ushaanza kuitwa kwa mungu.fanya mpango anza kugawa urithi.km mjomba wako alipewa cku 4 we umepewa 6.fanya tu uende kwa amani.au muulize mzee wa upako yule anae fufua watu halafu uwaulize wale waliofufuliwa kwamba inakuwaje huko wakuu.
Reply
Myakubanga
By Bujibuji:
Hebu tufanye umwiliisho (reinarnation) Reincarnation - Wikipedia, the free encyclopedia
Ahsante mkuu Bujibuji.
Sasa,ndio kusema pale wanakuwa wanaenda huko kwenye state ya unyama,spirip au ubinadamu mwingine?
Naomba unielezee vizuri kuhusu hyo reinarnation.
Reply
Defend or die
We acha tu nilipata tabu sana wakati wa kukata roho ni ngumu hiyo afadhali ukate mpingo kwa kiwembe.
Reply
albuluushiy
By Pasco:
Hii ni situation inaitwa "near death experience!" ambayo hutokea kabla ya kifo, wakati ambao roho inaacha mwili!.
Nitawahadithia kidogo experience yang na kuwapa za wengine!.
Niliwahi kupata ajali mbaya sana ya pikipiki, ikasemekana "nimekufa!", nikafunikwa kanga, na kuachwa wakisubiriwa polisi kufika kuuchukua mwili!. Kwa kawaida nikikumbuka huwa napata "stigmata" hivyo subirini nipate kidogo, ndipo nije nihadithie, ilikuwaje hatimaye nikawa hai tena1, na mpaka leo mimi nipo!.
Pasco.
una mambo wewe
Reply
SOURCE: JamiiForums.com