Ijumaa, 21 Juni 2013

Mimi nasema muwapige tu


: Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda.

Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda.
Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda.
 
Kauli ya waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda bungeni Dodoma katika mabishano kuhusu matumizi ya nguvu yanayofanywa na jeshi la Polisi nchini  humo ilitolewa bungeni alhamisi wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo kutoka kwa mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu .

Waziri mkuu huyo alijibu  “Ukifanya fujo umeambiwa usifanye hiki ukaamua wewe kukaidi utapigwa tu maana hakuna namna nyingine maana wote lazima tukubaliane nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria sasa kama wewe umekaidi hutaki unaona kwamba ni imara zaidi, wewe ndio jeuri zaidi watakupiga tu na mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine  maana tumechoka sasa”.


Nao wanaharakati wa haki za binadamu wamezungumza juu ya kauli hiyo Sauti ya Amerika ilizungumza na mtetezi  wa haki za binadamu Prugensi Massawe wa kituo cha sheria na  haki za binadamu  ambaye amehoji kauli hiyo ya waziri mkuu. Akielezea kila kitu kimeainishwa kwenye sheria kwasababu Tanzania ni nchi yenye utawala wa sheria.


Ripoti ya Mwamoyo Hamza

Nao wanaharakati wa haki za binadamu wamezungumza juu ya kauli hiyo Sauti ya Amerika ilizungumza na mtetezi  wa haki za binadamu Prugensi Massawe wa kituo cha sheria na  haki za binadamu  ambaye amehoji kauli hiyo ya waziri mkuu. Akielezea kila kitu kimeainishwa kwenye sheria kwasababu Tanzania ni nchi yenye utawala wa sheria.
Mahojiano na Prugensi Massawe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni