Jumapili, 14 Julai 2013

Ng`ombe waTaifa Stars hazai


Matumaini pekee ya nchi ya kucheza fainali za michuano ya kimataifa kabla ya 2015 yaliyobaki yalianza kuyeyuka jana baada ya timu ya Taifa Stars kufungwa 1-0 na majirani Uganda kwenye Uwanja wa Taifa.
Katika mechi hiyo ya kwanza ya kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani, CHAN, kwa mwaka 2014, bao la Uganda lilifungwa na Iguma Denis dakika moja baada ya mapumziko.
Kabla ya kufungwa jana, timu ya taifa ilikuwa imetoka kupoteza nafasi nzuri ya kuendelea kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia za Brazili za mwakani baada ya kufungwa na Ivory Coast 4-2 kwenye uwanja huo mwezi uliopita.
Kipigo cha mwezi uliopita kilikuja chini ya mwaka mmoja tangu Stars inyimwe nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, CHAN, za mwaka huu nchini Afrika Kusini na majirani wengine -- Msumbiji.
Stars na Uganda zitarudiana jijini Kampala wiki mbili zijazo katika mchezo ambao timu ya taifa ni lazima ishinde kwa angalau goli 1-0 ili kufufua matumaini ya kucheza fainali za CHAN kwa mara ya pili tangu 2009.
Kama ilivyokuwa katika mechi iliyopita ya Taifa Stars dhidi ya Ivory Coast, timu ya nyumbani ilitawala mchezo kwa muda mwingi wa kipindi cha kwanza lakini ikashindwa kubadili umiliki wa mpira kuwa magoli.
Ni udhaifu ambao uliadhibiwa vilivyo muda mfupi tangu kuanza kwa kipindi cha pili na wageni ambao walikuwa na wachezaji wawili tu wa Uganda Cranes A kutokana na kanuni za michuano hiyo kuibana.
Uganda ikipanga kikosi dhaifu, Tanzania ilianza na wachezaji tisa wa kikosi cha kwanza kutokana na kufaidika na ukosefu wa wachezaji wa ziada ya Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza soka nje ya mipaka ya nchi.
Timu zilikuwa:
STARS: Juma Kaseja, Erasto Nyoni (David Luhende dk.45), Shomari Kapombe, Agrey Moris, Kelvin Yondani, Frank Damayo, Amri Kiemba, Abubakar Salum, John Bocco, Mwinyi Kazimoto (Haruna Chanongo dk.56), Mrisho Ngassa.
UGANDA: Muwonge Hamza, Waswi Hassan, Wadada Nico, Majegwa Brian, Kabugo Savio, Kasaga Richard, Iguma Denis, Said Kyeyune, Mpande Joseph, Edama Patrick, Jur Tony

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni