Jumapili, 28 Julai 2013

Ripoti: Ubaguzi wa rangi Ulaya bado ni tatizo sugu


Shirika moja la kutetea haki za binadamu nchini Italia limesema kwenye ripoti yake kwamba, ubaguzi wa rangi barani Ulaya bado ni tatizo sugu. Shirika hilo linalojiita I CARE limesema tukio la hivi karibuni la kutupiwa ndizi waziri wa kwanza mweusi nchini humo limedhihirisha kuwa, ubaguzi wa rangi Italia na barani Ulaya kwa ujumla bado ni tatizo kubwa na lilanopaswa kukabiliwa vikali. Bi. Cecile Kyenge alitupiwa ndizi wakati akihutubia siku ya Ijumaa katika mji wa Cervia mkoani Ravenna, tukio linalonasibishwa na nyani au sokwe-mtu. Hii si mara ya kwanza kwa waziri huyo kukumbana na hujuma hiyo ya ubaguzi wa rangi. Miezi kadhaa iliyopita, Waziri Kyenge alizomewa na kundi la vijana mashariki mwa nchi hiyo na baadhi yao pia kumtupia ndizi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni