Jumatatu, 12 Agosti 2013

CUF yalaani waliomwagia tindikali wageni Zanzibar


Chama cha Wananchi, CUF, Zanzibar nchini Tanzania kimeelezea kushtushwa na tukio la kumwagiwa tindikali kwa raia wawili wa Uingereza katika maeneo ya Mji Mkongwe Zanzibar. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Salim Biman, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Habari, Uenezi, Mawasiliano na Umma imesema CUF inalaani kwa nguvu zote tukio hilo la kikatili la kuwamwagia tindi wageni hao ,na kinawataka polisi Zanzibar kufanya uchunguzi wa kina na waharaka pamoja na kuhakikisha kuwa wale wote waliohusika na tukio hilo la kikatili wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria. Taarifa ya Chama cha CUF imesema kama ninavyonukuu, “hii ni dalili mbaya kwa Zanzibar kwani matukio haya ya tindikali yamekuwa yanaonekana kama ni masuala ya kawaida jambo ambalo linatishia uchumi wa Visiwa vyetu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni